|
|
|
USIKILIZAJI wa kesi ya uhaini ya watu saba ambayo ilipangwa kuanza leo katika Mahakama Kuu, huenda ukahairishwa kwa sababu ya kutoelewana juu ya Mawakili watakaowatetea washitakiwa. Mpaka jana jioni ilikuwa haijajulikana ni nani atakayemtetea Michael Kamaliza. Bw. Kassam ambaye ndiye aliyekuwa amepangwa kumtetea tangu hapo awali amejitoa katika shughuli hiyo kwa sababu anakwenda ng’ambo kwa mafunzo zaidi. Bw. Talati, ambaye alichukua nafasi ya Bw. Kassam anasemekana kuwa ameondoka Dar es Salaam. Mwandishi wake aligoma kumweleza Mwandishi wa UHURU ni mahali gani alikokwenda ijapokuwa amesema atarejea baada ya siku mbili. Washitakiwa saba wanaokabiliwa na mashitaka ya makosa manne ya uhaini. Mashitaka yao yanaeleza vitendo mbalimbali vya uhaini na mojawapo ni kushirikiana na mkimbizi Oscar Kambona katika mpango wa kutaka kumuua Rais na kuipindua serikali halali ya Tanzania mnamo Oktoba mwaka jana. Mmoja wa washitakiwa hao, William Chacha ambaye mpaka hivi karibuni alikuwa Ofisa wa Mambo katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania katika Peking, inasemekana alidai kutoka kwa Kambona jumla ya shilingi milioni 20 kama bei ya kuipindua serikali ya Tanzania. Washitakiwa wengine ni Gray Likungu Mattaka (34), Mwandishi wa Habari, John Dustan Lifa Chipaka (38), Katibu Mkuu wa zamani wa chama marehemu cha African National Congress, Bibi Titi Mohammed (45), Rais wa zamani wa Umoja wa Wanawake, Michale Marshal Mowbray Kamaliza (46), Katibu wa zamani wa TANU na Waziri wa Kazi, Eliya Dustan Lifan Chipaka (32), Kapteni wa zamani wa Jeshi la Ulinzi na Alfred Philip Millinga (27), Luteni wa zamani wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania. Wote wamekanusha hatia ya mashitaka. Upande wa mashitaka utasimamiwa na Mwanasheria Mkuu wa serikali Bw.
Mark Bomani, akisaidiwa na Makamu wa Mwanasheria Mkuu.
|
YALIYOMO
Tahariri Baada ya futari nzuri: Tuwatupie macho wenye njaa Rais Mkapa kuwa mgeni rasmi Baraza la Idd Waumini, Masheikh Arusha wasutana kwa futari ya Mrema Dondoo za saikolojia
MSADAT yazidi kutia moyo Tanga MAFUNZO KUHUSU FUNGA YA RAMADHANI Michezo isiyoruhusiwa katika Uislamu Ustadh Farid: Kijana aliyejitolea kuwapa Da'awa watalii Hakuna Magharibi wala Mashariki:
Uislamu ni ubinaadamu
Ijue madrasati Mar-wa ya Dodoma
mjini
Ijue Madrasat Jadidul Fiqhyyat
- Tabata Kimanga
Madrasat Hidayatul Muumini Mwadui Washindi wa mashindano ya Hadithi za Mtume (s.a.w.) wapatikana Madrasa Shafii Ujiji Kigoma yaonyesha umahiri wake Waanzisha mifuko kusaidia wagonjwa Dodoma Waislamu Kondoa waomba msaada kumalizia Msikiti Mnyororo wa imani-2
Kutoka magazeti ya zamani:
Jengo la Waislamu Moshi lageuzwa
Kanisa la Walokole
Masjid Nurania yaswaliwa
Ijumaa
Jabal Hira kutoa mafunzo
ya Kompyuta Morogoro
Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|