AN-NUUR 
Na.184 Ramadhan 1419, Januari 15 - 21, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Washindi wa mashindano ya Hadithi za Mtume (s.a.w.) wapatikana
  

Washindi wa mashindano ya Hadithi za Mtume Muhammad(S.A.W.) yaliyo andaliwa na Africa Muslims Agency wamepatikana.  

Washindi hao ni: Abdi Kassim Jiba wa Daarul-Hadiith Assalafiyya ya Tanga Aliyeshika nafasi ya kwanza na alijipatia Shilingi.75,000/-, Cherehani na kitabu cha Sahiih Bukhaariy. 

Aliyeshika nafasi ya pili ni Ibrahim Kibwana kutoka Madrasatul-Azhar ya Dar es Salaam na alijipatia Shilingi .50,000/, Radio Cassette na kitabu cha Sahiih Bukhaariy 

Ally Jumanne wa Ma’had Ansaar Sunna ya Arusha alishika nafasi ya tatu na alijipatia Shilingi 25,000/= na Fani ya wima. 

Aidha washindani wote kumi walio shiriki katika mashindano hayo walipata zawadi za vitabu, boksi moja la tende na shuka (saruni). 

Mashindano hayo yalishirikisha vijana kumi kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Arusha na Iringa na yalifanyika Desemba 5, 1998 katika ukumbi wa Star Light Jijini Dar es Salaam. 

Akitoa nasaha zake katika mashindano hayo, mgeni rasmi Sheikh Abdulqadir Juneid alilipongeza Shirika la Africa Muslims Agency kwa kuandaa mashindano hayo na pia aliwapongeza vijana washindani kwa uwezo wao mkubwa walio uonyesha wa kuhifadhi, kufahamu na kuzichambua Hadithi. 

Naye Mkurugenzi wa Africa Muslims Agency Bw. Abderraheem Ben-Ainouss akizungumza katika mashindano hayo alisema kuwa Shirika lake limeandaa mashindano hayo ya Hadithi ili kuikumbusha jamii ya Kiislamu juu ya umuhimu wa Hadithi ambazo ndio chimbuko la pili la sheria za Kiislamu baada ya Qur’ani. 

Aidha mratibu wa mashindano hayo Sheikh Mbwana A. Urari aliwashukuru wale wote walio fanikisha mashindano hayo na hasa wale walio toa zawadi kwa washindani. 


Madrasa Shafii Ujiji Kigoma yaonyesha umahiri wake

WANACHUONI 58 wa madrasati Shafii ya Ujiji katika Halmashauri ya mji wa Kigoma hivi karibuni walifanya maonyesho ya masomo siku ya kufunga chuo hicho ambacho ni tawi la madrasati Muumin kwa ajili ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. 

Katika sherehe hiyo wanachuo walifanya maonyesho ya Hadith, Sira pamoja na sheria na mashairi kuhusu dini ya Kiislamu, mafunzo ambayo yalilenga katika kujenga uadilifu kwa Waislamu mbele ya Mwenyezi Mungu. 

Mwajuma Yasin (14) alianza kwa kuwakumbusha Waislamu ubora wa kufunga katika mwezi mtukufu wa Ramadhani ambayo ni nguzo ya nne kati ya nguzo tano za dini ya Kiislamu. 

Mwanachuo huyo alisema Muislamu katika kufunga anatakiwa ajizuie kula, kunywa na pia kuacha kukutana kimwili kati ya mke na mume wakati wa mchana kama njia ya kuonyesha utii mbele ya Mwenyezi Mungu. 

Mwanachuo mwingine Zuhura Mwamadi (13) aliwaasa Waislamu kutoshiriki katika kunywa pombe, kinywaji ambacho kimeharamishwa na Mwenyezi Mungu, kwani ni chanzo kikubwa cha kuchochea maasi. 

Aidha, wakati wa maonyesho hayo yaliyohudhuriwa na wazazi wa wanachuo, wanachuo wengine waliotoa nasaha zao kupitia aya mbalimbali ni pamoja na Sungura Ruti (14) aliyewataka Waislamu kuitafuta elimu na baadaye kuieneza kwa wenzao ili kusaidia maendeleo yao. 

Sungura alitoa mifano ya elimu kama vile useremala, kushona na kufuma nguo, kuwafundisha Waislamu ufasaha mambo yaliyoamrishwa kufanywa na Mwenyezi Mungu ikiwa ni pamoja na yaliyokatazwa kwa kutumia vitabu vya dini. 

Mwanachuo Sango Mwamadi na Zawadi Abdallah nao waliwataka Waislamu kutofurahia kuona machafu, yaani madhambi, mfano kutukana na kusengenya pamoja na kuwaheshimu wazazi kama alivyoamrisha Mtume Muhammad (s.a.w.). 

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mara baada ya maonyesho hayo, mwalimu wa madrasa hiyo Ustadh Jalaleni Ramadhani aliwakumbusha baadhi ya wazazi ambao huchelewa kulipa ada, kufanya hivyo bila kuathiri utaratibu wa chuo hicho. 

 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Tahariri 
Baada ya futari nzuri: Tuwatupie macho wenye njaa 

Rais Mkapa kuwa mgeni rasmi Baraza la Idd 

Ubungo yakumbwa na ukame 

Waumini, Masheikh Arusha wasutana kwa futari ya Mrema 

Dondoo za saikolojia 
Na. Abu Halima Sa Changwa 

Waislamu turejee kwa Allah 

MSADAT yazidi kutia moyo Tanga 

Mjue Usama bin Ladin 

MAFUNZO KUHUSU FUNGA YA RAMADHANI 

Michezo isiyoruhusiwa katika Uislamu 

Ustadh Farid: Kijana aliyejitolea kuwapa Da'awa watalii 

Hakuna Magharibi wala Mashariki: Uislamu ni ubinaadamu 
Na Abubakari S. Marwillo 

Ijue madrasati Mar-wa ya Dodoma mjini 
Na Abu Zuberi, Dodoma 

Ijue Madrasat Jadidul Fiqhyyat - Tabata Kimanga 
Na B. Mwakangwale 

Madrasat Hidayatul Muumini Mwadui 

Washindi wa mashindano ya Hadithi za Mtume (s.a.w.) wapatikana 

Madrasa Shafii Ujiji Kigoma yaonyesha umahiri wake 

Waanzisha mifuko kusaidia wagonjwa Dodoma 

Waislamu Kondoa waomba msaada kumalizia Msikiti 

Mnyororo wa imani-2 
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa 

Kutoka magazeti ya zamani: 
Wanaoshitakiwa kwa uhaini kortini leo 

Jengo la Waislamu Moshi lageuzwa Kanisa la Walokole 
Na Mwandishi Wetu, Moshi 

Masjid Nurania yaswaliwa Ijumaa 
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Jabal Hira kutoa mafunzo ya Kompyuta Morogoro 
Rajab Rajab na Mussa Ally, Morogoro 

Sayansi na Teknolojia 
[Internet ni nini?] 

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Thamani ya mlo wa Uyoga] 
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita