AN-NUUR 
Na.184 Ramadhan 1419, Januari 15 - 21, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Mnyororo wa imani-2
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa

Sasa tuone Manabii wamekiheshimu vipi kiapo hicho cha kiroho. Nabii Daud (a.s.) anasema: "Neno la BWANA kwa Bwana wangu, uketi mkono wangu wa kuume. Hata niwafanyapo adui zako kuwa chini ya miguu yako". (Zaburi 110:1. Na Nabii Yesu (a.s.) akitamba na filosofia yake ya juu, anawajaribu wasomi wa Kiyahudi kwa kuwaambia: "Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akasema, mwaonaje katika habari za Kristo? Ni mwana wa nani? Wakamwambia, ni mwana wa Daud. Akawauliza, imekuwaje basi Daud katika Roho kumwita Bwana, akasema, Bwana alimwambia, Bwana wangu umeketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako kuwa chini ya miguu yako. Basi Daud akamwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe? Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu yeyote tangu siku ile kumwuliza neno tena". (Mathayo 22:41-46). 

Wanatheolojia wa sasa wakijaribu kujibu swali hilo, nao wanavurunda kabisa kusema: "22:45 Masiya, ingawa ni nasaba ya Daud kadiri ya ukoo wake wa kibinadamu (1:1-17), alikuwa na tabia ya kimungu pia iliyomfanya awe juu ya Daud. Na hali hiyo Daud alikwisha isema mbele. Hilo ndilo jibu walilopaswa kumpa Yesu". (Biblia takatifu Tabora Uk. 901). 

Nabii Yesu (a.s.) akimtukuza Nabii Yohana (a.s.) kuliko Manabii wote waliokuwa kabla yake anasema "Amin, nawaambieni, Hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji ..." (Mathayo 11:11). Lakini akilimlinganisha na yeye (Yesu a.s.) anamalizia kwa kusema "... walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye (Yohana a.s.). Akithibitisha hilo, Yohana (a.s.) anasema "kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba, bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto". (Mathayo 3:11). Yohana (a.s.) alimwogopa Yesu (a.s.) hata kabla Yesu hajapewa utume. "Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordan kwa Yohana ili abatizwe. Lakini Yohana alitaka kumzuia, akisema, mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu? Yesu akajibu akamwambia, kubali hivi sasa, kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote. Basi akamkubali (Mathayo 3:13-15) na Mtume atakayekuja baada yake, alisalimu amri na kusema "Mimi sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa maana yuaja MKUU wa ulimwengu huu, wala hana kitu kwangu". (Yohana 14:30). 

Tazama pia Mathayo 12:31-32. Hapa napenda niweke wazi kuwa, neno "ulimwengu" hapo halimaanishi milki ya shetani. Kwani shetani anaimiliki dunia tangu enzi za Adam na Hawa. Hivyo Yesu (a.s.) asingetumia neno "yuaja" kama angemaanisha shetani. Neno "ulimwengu" limefasiriwa na wanatheolojia kama ifuatavyo: "1:9 "Ulimwengu" kadri ya Yohana una maana au ya viumbe vyote au ya dunia au binadamu au wale wote wanaomkataa Mungu na kumdhulumu Yesu Kristo na wafuasi wake (7:7; 18:19; 17:14). Anaposema "ninyi ni wa ulimwengu huu" au kitu kama hicho Yohana anatumia maana hiyo ya mwisho ya ulimwengu (8:23) Biblia Takatifu Tabora Uk. 967. Hivyo neno "mkuu wa ulimwengu" linamaanisha mkuu wa dunia yote na vilivyomo. Yaani Nabii Mkuu. 

Ili mtu ajue Mwenyezi Mungu anataka nini na kwa utaratibu gani katika wakati uliopo, lazima akubali kufanya "kazi ya Mungu". "Basi wakamwambia, tufanyeje ili tupate kuzitenda kazi za Mungu? Yesu akajibu, akawaambia, Hii ndio kazi ya Mungu, mwaminini Yeye aliyetumwa na Yeye". (Yohana 6:28-29). 

Kutokumwamini Mtume aliyetumwa katika wakati unaohusika ni kumchukiza sana yule Mtume unayemwamini. Hili limewekwa wazi na Mtume Yesu (a.s) "Msidhani kwamba mimi nitawashitaki kwa Baba, yuko anayewashitaki, ndiye Musa mnayemtumaini ninyi. Kwa maana kama mngalimwamini Musa, mngeniamini na mimi, kwa sababu yeye aliandika habari zangu. Lakini msipoyaamini maandiko yake, mtayaamini wapi maneno yangu". (Yohana 5:45-47). 

Hivyo, kumkataa, kumdharau, kumtukana Mtume aliyekuja baada ya Mtume unayemwamini ni madhambi makubwa sana. Jitihada yoyote mtu atakayofanya ili kuhalalisha matusi yake, inathibitisha uduni wake wa fikra na kubobea kwa kiasi kikubwa katika fani ya upuuzi, uzushi na porojo. Na jinsi mtu atakavyokazana kufanya juhudi hiyo, ndivyo anavyodhihirisha ubingwa wake katika fani hiyo. Cha kushangaza sana waliobobea sana katika fani hiyo ni Maprofesa. Katika kuthibitisha ubingwa wao, wanatuletea kitabu kiitwacho "Allah wa kwenye Qur’an siye Yehova". Mimi kabla sijasoma kitabu hicho, nacho nakiita cha upuuzi (Rejea makala yangu "Msiiparamie ovyo Biblia" katika ANNUUR Na. 169). 

Ndugu msomaji hebu fuatilia maelezo ya Kamusi zifuatazo nadhani nawe utaniunga mkono. Katika Kamusi iitwayo "Alqamus al Madrasi - The Dictionary". Arabic - English, English - Arabic ya Bwana Elias A. Elias, 1984, Karachi Pakistan ikifasiri neno "Mwenyezi" katika Uk. 10 inasema "Almighty - Alqadiir Alqadiiru alaa kullli shay-in" (yaani, mwenye uwezo. Mwenyezi uwezo wa kila kitu). Ikifasiri neno "Mungu" katika uk. 131 inasema "God - Allah. Ilaaha, Rabbbu" (yaani, Mwenyezi Mungu. Mungu Bwana). Hapa tuzingatie kwamba; neno "Jehova" ni neno la Kiebrania. Hivyo halimo katika kamusi ninazotumia hapa za Kiingereza, Kiarabu na Kiswahili. Badala yake tunatumia neno lililo sawa nalo la "Mwenyezi Mungu" (tazama Biblia Uk. VI). 

Sasa tuzingatie kamusi nyingine iitwayo "A Standard Swahili - English Dictionary" ya iliyokuwa Inter-territorial Language Committee for the East African Dependencies chini ya Katibu wake Mkuu Frederick Johnson iliyotolewa na Oxford University Press, Ely House, London W.I., mwaka 1939. Kamusi hii imepata baraka za Askofu Thomas wa Zanzibar na ndiye aliyeiandikia neno la awali (fore word). 

Pamoja na maneno mengine ya kuisifu anasema: "It is a matter of good fortune that the revision of these two dictionaries (Za steere na Madan) was placed in the capable hands of the late Frederick Johnson, formerly Secretary of the Inter-territorial Language (Swahili) Committee, which has done so much so standardize the language and to preserve its orthography from confusion (kama hizi za Maprofesa). Anamalizia kwa kusema "This conspectus of the Swahili language neill there fore help us all to find that the language is more worthy of our serious study than perhaps we had previously considered". 

Katika ukurasa wa 9-10 tunakuta maneno "Allah - n. God. Seldom used except in Arabi expressions and formulas, such as: Allah Akbar, God is great. La illahi ila Allah, there is no God but God, the first clause of Muhammadan creed, which is song over and over again by the funeral procession on its way to the grave ... (cf. Rasi, Mola, Mungu. Ar.). Katika ukurasa wa 315 tunakuta maneno "Mungu, n. (miungu). (1) God, a god; (2) Providence, luck, accident - used to describe anything unccountable or unexpected. Words connected with Mungu are Mwenyezi Mungu, i.e. Mwenye enzi Mungu, Almighty God... Mola is sometimes used for God, but Seldom Allah ... (cf. Mola, Allah, Rabi, and various titles of God)" 

Ili nami nitoe mchango wangu wa "kufanikisha" kitabu hicho (Allah sio Yehova), naona nimwongezee Profesa wangu maneno Kristo, Isa, Nabii na Mtume kwa mujibu wa kamusi hizo. 

Katika kamusi ya Elias A. Elias Uk. wa 49 tunakuta maneno "Christ - Assayyidul Masiihu. Isa" (Kristo - Bwana masihi. Isa). Na katika kamusi ya Frederick Johnson Uk. 143 tunakuta maneno "Isa, n. a Proper name. Also the name for Jesus Christ known to Muhammadas - often with addition bin Mariam. Katika Uk. 328 tunakuta maneno "Nabii, n. ma- a Prophet, a preacher of righteousness, one who foretells the future. Used of Adam, Noah, Abraham, Jesus, and others as well as Muhammad. (cf. bashiri, tabiri, sibu. 

Na katika ukurasa wa 477 tunakuta maneno "... Mtume, n. one who is employed or sent, a messenger, an emissary, but esp. Muhammad. i.e. Apostle, and also of the chief characters of the old testament, Moses, Job, and others. It is the word adopted for Christian Apostles also ... used like Mtume, of Muhammad, as Apostle of God...". 

Namalizia kwa kusema, ninakisubiri kitabu hicho kwa hamu. 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Tahariri 
Baada ya futari nzuri: Tuwatupie macho wenye njaa 

Rais Mkapa kuwa mgeni rasmi Baraza la Idd 

Ubungo yakumbwa na ukame 

Waumini, Masheikh Arusha wasutana kwa futari ya Mrema 

Dondoo za saikolojia 
Na. Abu Halima Sa Changwa 

Waislamu turejee kwa Allah 

MSADAT yazidi kutia moyo Tanga 

Mjue Usama bin Ladin 

MAFUNZO KUHUSU FUNGA YA RAMADHANI 

Michezo isiyoruhusiwa katika Uislamu 

Ustadh Farid: Kijana aliyejitolea kuwapa Da'awa watalii 

Hakuna Magharibi wala Mashariki: Uislamu ni ubinaadamu 
Na Abubakari S. Marwillo 

Ijue madrasati Mar-wa ya Dodoma mjini 
Na Abu Zuberi, Dodoma 

Ijue Madrasat Jadidul Fiqhyyat - Tabata Kimanga 
Na B. Mwakangwale 

Madrasat Hidayatul Muumini Mwadui 

Washindi wa mashindano ya Hadithi za Mtume (s.a.w.) wapatikana 

Madrasa Shafii Ujiji Kigoma yaonyesha umahiri wake 

Waanzisha mifuko kusaidia wagonjwa Dodoma 

Waislamu Kondoa waomba msaada kumalizia Msikiti 

Mnyororo wa imani-2 
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa 

Kutoka magazeti ya zamani: 
Wanaoshitakiwa kwa uhaini kortini leo 

Jengo la Waislamu Moshi lageuzwa Kanisa la Walokole 
Na Mwandishi Wetu, Moshi 

Masjid Nurania yaswaliwa Ijumaa 
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Jabal Hira kutoa mafunzo ya Kompyuta Morogoro 
Rajab Rajab na Mussa Ally, Morogoro 

Sayansi na Teknolojia 
[Internet ni nini?] 

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Thamani ya mlo wa Uyoga] 
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita