|
|
|
KAMA ilivyo kawaida ya kila mwaka viongozi wa ngazi za juu serikalini Ramadhani hii wamewaandalia futari Masheikh na baadhi ya wazee mashuhuri jijini Dar es Salaam. Japo futari hii huandaliwa mara moja tu kwa mwezi, lakini ina ujumbe mzito zaidi ya chakula chenyewe. Kwanza ni kujenga maelewano, mapenzi na udugu kama Mtume (s.a.w.) alivyousia kwamba: "Alikaneni (kwa chakula n.k.) mtapendana". Pili na kubwa zaidi ni zile fadhila na thawabu anazozipata muumini anapomfuturisha Muislamu mwenzake aliyefunga. Japo si Waislamu wote waliopata fursa ya kufuturishwa Ikulu au kwa Mh. Makamu wa Rais; lakini ule udugu na kutakiana kheri kuliko onyeshwa hapana shaka kunakusudiwa kwa Waislamu wote. Yeyote mwenye kutoa sadaka kwa imani na ikhlasi huichunga sadaka yake isiruke patupu. Haifuatilii kwa maneno ya kero na adha. Na yeyote aliyehiji Hija Mabrur haitii matope hija yake anaporejea. Ni matarajio yetu kwamba baada ya kupeana futari nzuri tutapeana pia mkono wa kheri wa Idd el Fitr. Hatutarajii leo tufuturu pamoja kwa furaha siku mbili baadae tena furaha yote ya Eid itumbikie nyongo kwa kauli zetu za masimango na kejeli. Siku ya Eid el Fitr ni siku adhim ni siku ya furaha, siku ya kula na kunywa vilivyo vizuri basi tupeane fursa ya kusherehekea. Tupeane kauli njema; tupongezane na tupeane nasaha za matarajio mema. Wakati wengine tukila futari kwa wasaa, vyombo vya habari vinaarifu kwamba huko Kilwa wanafuturu embe. Basi hawa nao tuwazingatie na tuwahurumie. Moja ya mafunzo ya funga ni kutupa fursa kupata hisia azipatazo ashindae na njaa kwa umasikini wake. Kama tunaweza kuwafuturisha wenzetu ambao tangu hapo wana uwezo wa kujifuturisha; kama ishara ya kuonyesha udugu na mapenzi miongoni mwetu; basi udugu huo unastahiki tuuonyeshe zaidi kwa hawa wenzetu wafuturuo embe. |
YALIYOMO
Tahariri Baada ya futari nzuri: Tuwatupie macho wenye njaa Rais Mkapa kuwa mgeni rasmi Baraza la Idd Waumini, Masheikh Arusha wasutana kwa futari ya Mrema Dondoo za saikolojia
MSADAT yazidi kutia moyo Tanga MAFUNZO KUHUSU FUNGA YA RAMADHANI Michezo isiyoruhusiwa katika Uislamu Ustadh Farid: Kijana aliyejitolea kuwapa Da'awa watalii Hakuna Magharibi wala Mashariki:
Uislamu ni ubinaadamu
Ijue madrasati Mar-wa ya Dodoma
mjini
Ijue Madrasat Jadidul Fiqhyyat
- Tabata Kimanga
Madrasat Hidayatul Muumini Mwadui Washindi wa mashindano ya Hadithi za Mtume (s.a.w.) wapatikana Madrasa Shafii Ujiji Kigoma yaonyesha umahiri wake Waanzisha mifuko kusaidia wagonjwa Dodoma Waislamu Kondoa waomba msaada kumalizia Msikiti Mnyororo wa imani-2
Kutoka magazeti ya zamani:
Jengo la Waislamu Moshi lageuzwa
Kanisa la Walokole
Masjid Nurania yaswaliwa
Ijumaa
Jabal Hira kutoa mafunzo
ya Kompyuta Morogoro
Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|