AN-NUUR
Na.158 Rabi' Awal 1419, Julai 17 - 23, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 MASHAIRI

Nyoka mleleka  

Bismillahi hakika, ninaanza kuandika, 
Kwa jina lake Rabbuka, ambae ametukuka, 
Naomba zake baraka, kadiri atavyotaka, 
Wazee kufuga nyoka, nyoka si wa kufugika. 

Wazee twawakumbuka, wengine wametutoka, 
Wamekwenda kwa Rabbuka, siku zilipowafika, 
Majina sintotamka, huzuni imenishika, 
Wazee kufuga nyoka, nyoka si wa kufugika. 

Walichofanya hakika, ni wema waliutaka, 
Ndipo walipomshika, kuona ahangaika, 
Nyoka akakamatika, kawa mwana ‘Mleleka’ 
Wazee kufuga nyoka, nyoka si wa kufugika. 

Ndani wakaja muweka, kwa furaha na kucheka, 
Wakatandika mikeka, kumkaribisha nyoka, 
Kisha akafukuzwa paka, aondoke kwa haraka, 
Wazee kufuga nyoka, nyoka si wa kufugika. 

Chakula wakakipika, “Karamu” wakaandika, 
Wakamfariji nyoka, mwana asiye na kaka, 
Kila alichokitaka, kwake kikakamilika, 
Wazee kufuga nyoka, nyoka si wa kufugika. 

Nyoka alipozinduka, kwamba “uemi” ataka, 
Kisha ameaminika, wazee hawana shaka, 
Ndipo alipotamka, Baleghe imeshafika, 
Wazee kufuga nyoka, nyoka si wa kufugika. 

Wazee bila ya shaka, wala inda kutendeka, 
Mambo yakatimizika, na fedha zikachangika, 
Ulaya kukaendeka, kafaulu mwana nyoka, 
Wazee kufuga nyoka, nyoka si wa kufugika. 

Alipovuka mipaka, kuacha Afrika, 
Akaomba kwa Rabbuka, ili salama kufika, 
Na huko alipofika, mikakati  akaweka, 
Wazee kufuga nyoka, nyoka si wa kufugika. 

Mikakati aloweka, kawambia wahusika, 
Kwamba anachokitaka, ni mwitu aliotoka, 
Akabidhiwe waraka, atawale Tanga na nyika, 
Wazee kufuga nyoka, nyoka si wa kufugika. 

Hilo halikupingika, kwa hao wahusika, 
Ila walilomtaka, awe wao ‘kibaraka’, 
Na ipate enezeka, itikadi ya mashaka, 
Wazee kufuga nyoka, nyoka si wa kufugika. 

Kakabidhiwa waraka, akarudi kwa haraka, 
Kajaza anavyotaka, ndugu zake wa Ki-nyoka, 
Msitu akaushika, kadhibiti madaraka, 
Wazee kufuga nyoka, nyoka si wa kufugika. 

Hatamu aliposhika, sheria zikatungika, 
Hakuna wa kutamka, kupinga anavyotaka, 
Nyoka wasohesabika, wakazunguka mipaka. 
Wazee kufuga nyoka, nyoka si wa kufugika. 

Yeyote alohisika, kuhoji mambo ya nyoka, 
Ndani kasahaulika, na kifo kikamfika, 
\Sumuye haina shaka, inaua kwa haraka, 
Wazee kufuga nyoka, nyoka si wa kufugika. 

S.M. SAIDI  LINZE, 
Masjid Nuur, 
S.L.P. 116, 
MPANDA. 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI  

Maoni yetu: Wananchi kataeni kupotoshwa 

SUALA LA MWEMBECHAI: Wabunge wataka kujua nani aliamrisha kuua 
Na Mwandishi wetu  

Katiba ya nchi yapuuzwa: Waislamu wapigwa marufuku kuhubiri  

Mtihani darasa la saba 1998: Manispaa Moro yaagiza ipewe majina ya wanafunzi Wakatoliki 
Na Rajab Rajab, Morogoro 

 “Wushu”ya Waislamu wa China na jinsi ilivyowasaidia kupambana na dhulma dhidi yao 
Na MUSSA ALLY  

Yesu wa kwenye Mathayo siyo Yesu wa kwenye Luka 
Na. Masoud Mohammed 

Ni nani hawa Waislamu wa Siasa Kali ? 
Na USTADH  A.S. FUNDI  

Waislamu tuondokane na unyonge 
Na Abubakar Marwilo 

Maisha ya ndoa kwa Mwislamu 

Waislamu wana mwelekeo wao 
Na Sheikh Pandukizi Dilunga 

Ni mwaka gani Yesu alianza kuitwa Mungu 
Na MCHUNGAJI A.T. MANONI  

Wanawake wameamua kuwa wazi kweli kweli 
Na Bi. Fatma Musa 

Kimya kingi kina mshindo mkuu: Vipi Mhe. Rais wale walioua? 
Na Mussa Ally 

Mtazamo wa madhalimu wa Tanzania kwa Waislamu 
Na Rajab Isa 

Aliyoyasema KK bungeni 

Waislamu mkoa wa Morogoro wampinga Yahya 
Na. Abu Adli  

Polisi wachafua mazingira ya msikiti wa Mwembechai 
Na Badru Kimwaga 

Wanawake wa Kiislamu Ubungo darajani wamuunga mkono Sheikh Bafadhil 
Na Kassim Juma 

Barua za wasomaji  

Mashairi  

Mafundisho ya Qur'an: Kanuni za kumkumbuka Allah na kutumia katika njia yake 

Masomo  

Chakula na lishe: Lishe ya mtoto aliyekuwa mgonjwa 
Na Mujahiid Mwinyimvua 
 

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita