|
|
|
Lishe ya mtoto aliyekuwa mgonjwa Na Mujahiid Mwinyimvua WAKATI mtoto (au mtu mzima) anaugua, mwili wake unapoteza viinirishe vingi, kwa mfano vitamini A na madini ya chuma. Vitamini A inasaidia kuupa mwili kinga na pia inasaidia macho kuona vizuri. Madini ya chuma yanatumika mwilini kutengeneza damu. Kutokana na kupotea kwa viinirishe (virutubisho) mwilini, mtoto (au mtu mzima) aliyetoka katika ugonjwa, huwa na njaa kuliko ilivyo kawaida. Kwahiyo, huwa anakula sana na kukua kwa haraka kuliko ilivyo kawaida mpaka mwili wake utakaporudia hali yake ya kawaida, vile ulivyo. Kipindi hiki kwa kimombo kinaitwa ‘catch –up growth’ kwa lugha yetu ya Kiswahili tunaweza kukiita kipindi cha kufidia makuzi yaliyoathiriwa kwa sababu kadhaa, mojawapo ni maradhi. Kipindi hiki cha kufidia makuzi pia hupatikana kwa watoto waliokuwa na minyoo. Kwa maneno mengine, watoto wenye minyoo, huwa wanamahitaji makubwa ya chakula hasa baada ya minyoo aliyokuwa nayo kuuliwa kwa dawa. Baadhi ya wazazi hukasirika kuwaona watoto wao wanakula zaidi kuliko ilivyo kawaida hasa wanapotoka katika maradhi. Tabia kama hii si nzuri, hivyo basi nawaomba wazazi wenzangu wawape chakula kizuri, safi, salama na cha kutosha watoto (au watu wazima) waliotoka katika maradhi. Hii ni kwa sababu watoto waliokuwa wagonjwa wasipopatiwa mlo wa kutosha, miili yao haitaweza kufidia kwa haraka virutubisho vilivyoharibika au vilivyopea. Hali hiyo inaweza kuchangia ugonjwa kurudi au mwili wa aliyekuwa mgonjwa kuzidi kuwa dhaifu na kuathiri ukuaji wa mtoto kwa ujumla. Watoto waliotoka katika maradhi ambao bado wananyonya, wanyonyeshwe maziwa ya mama mara nyingi, hata zaidi ya mara kumi na tano katika kipindi cha saa 24. Watoto hao kama wana umri zaidi ya miezi minne waongezewe chakula kinachostahiki kwa umri wao. Somo hili tulishalizungumza katika makala zetu zilizopita. Watoto au watu wazima waliokuwa wagonjwa wapewe vyakula mchanganyiko (wanga, protini,vitamini, maji, madini, nyuzi nyuzi, n.k.). Pia lazima wapewe vyakula vyenye sifa maalumu ya kujenga na kulinda mwili. Vyakula hivyo ni kama vile nyama, samaki, maziwa, maini, mayai, embe, mafuta, siagi (margarine) mboga za majani, nanasi, uyoga, n.k. Hata hivyo, ni vyema ikakumbukwa kuwa, vyakula vilivyotajwa hapo juu vina kanuni yake. Kwa mfano, ni hatari kwa afya kuweka mafuta au siagi nyingi katika chakula. Mafuta yanayotokana na mimea ni salama zaidi kwa afya kuliko yale yanayotokana na wanyama. Kanuni nyingine ya vyakula ni kuwa mayai si chakula kizuri kwa watoto
wadogo (chini ya miaka miwili) kwa sababu yana mafuta ya hatari "cholesterol",
hivyo basi mtoto mdogo apatiwe vyakula vingine vyenye protini kwa wingi
kama vile maziwa, maini n.k.
|
Maoni yetu: Wananchi kataeni kupotoshwa SUALA LA MWEMBECHAI: Wabunge
wataka kujua nani aliamrisha kuua
Katiba ya nchi yapuuzwa: Waislamu wapigwa marufuku kuhubiri Mtihani darasa la saba 1998: Manispaa
Moro yaagiza ipewe majina ya wanafunzi Wakatoliki
“Wushu”ya Waislamu wa China
na jinsi ilivyowasaidia kupambana na dhulma dhidi yao
Yesu wa kwenye Mathayo siyo Yesu wa
kwenye Luka
Ni nani hawa Waislamu wa Siasa Kali
?
Waislamu tuondokane na unyonge
Waislamu wana mwelekeo wao
Ni mwaka gani Yesu alianza kuitwa
Mungu
Wanawake wameamua kuwa wazi
kweli kweli
Kimya kingi kina mshindo mkuu:
Vipi Mhe. Rais wale walioua?
Mtazamo wa madhalimu wa Tanzania
kwa Waislamu
Waislamu mkoa wa Morogoro
wampinga Yahya
Polisi wachafua mazingira
ya msikiti wa Mwembechai
Wanawake wa Kiislamu Ubungo
darajani wamuunga mkono Sheikh Bafadhil
Mafundisho ya Qur'an: Kanuni za kumkumbuka Allah na kutumia katika njia yake Chakula na lishe: Lishe ya
mtoto aliyekuwa mgonjwa
|