|
Na. 060 Jumatano Agosti 9 - 15, 2000 |
|
|
|
|
|
Ulaji wa matunda Na Mariamu M. Mbwambo MATUNDA ni mojawapo katika vihitajio muhimu sana katika kulinda mwili wa binadamu. Ingawa watu wengi ulaji wao wa matunda ni wa nadra kwa kutokufahamu umuhimu na faida zinazopatika kwenye matunda. Natuone basi baadhi ya faida na matumizi ya matunda. Matunda kwa ujumla hutupatia proteni kwa kujenga mwili, mafuta kwa ajili ya kuupa nguvu mwili,mafuta hupatikana kwa wingi kwenye maparachichi, tunapata wanga katika muundo wa sukari. Pia vitamini C ambayo ipo katika kiwango kikubwa sana. Vile vile matunda yana madini kama "kalsiam" madini ya chuma, asidi ya matunda ambayo hupatikana zaidi kwenye "citrus fruits" kama malimao, machungwa n.k. Maji yaliyomo kwenye matunda ni kama asilimia themanini na tano . Matunda yanafaa yaliwe yakiwa yameoshwa na katika hali ya kuvutia, yasiwe yenye madoadoa na yenye kuonyesha kukaa zaidi ya kufikia kupoteza virutubisho muhimu vihitajikavyo mwilini. Pia ni vizuri matunda kuliwa/kuchaguliwa unaponunua yakiwa yameiva,kwani matunda mabichi huwa magumu kuyeyushwa kwa urahisi tumboni (DIGESTIoN) kutokana na asidi iliyomo humo. Pia ni vizuri matunda yakatumiwa yakiwa kwenye msimu na yahifadhiwe vizuri yasiharibike. Baadhi ya matunda yanaweza kupikwa na kutumwika kama chakula,mfano wa hayo ni ndizi mbichi, hii husaidia kulainisha matunda hayo ili yaweze kusagwa kwa urahisi tumboni. Pia matunda yanapopikwa husaidia kuyahifadhi na kukaa kwa muda mrefu, vilevile bakteria waliomo kwenye matunda hayo hufa. Matunda mengine huliwa yakiwa yamemenyewa au na maganda yake. Haya ni kama maembe, ndizi, machungwa,tikiti maji, papai na mananasi, kwa lugha ya kigeni matunda haya yanajulika kama (SERVING FRUITS). Matunda yana kazi kubwa katika kuilinda miili yetu isipatwe na magonjwa.Hivyo basi matumizi haya hutegemea sana asili ya tunda hilo, mfano ndizi itakapochanganywa na unga wa ngano na kutengenezwa mkate itatumika kama kitafunwa yaani (SNACK) na inaweza kutumika kutengeneza juisi itakapochanganywa na maziwa. Pamoja na hayo kuna baadhi ya matunda huweza kutengenezewa supu mfano nyanya, jhamp, vinywaji kama juisi, viungio vya mboga kama limao, pia matunda huweza kuchanganywa pamoja katika vipande vyembamba na vidogo vidogo kama salad. Hivyo basi tunashauriwa kutumia matunda ipasavyo hasa kwa watoto, watu wazima pamoja na watu wote kwa ujumla ili kuchangamsha mfumo mzima wa neva,vilevile kuilinda miili yetu na magonjwa. |
YALIYOMO
KAULI
YA WAISLAMU
Karume adaiwa ‘kutafuta ujiko’ kwa kutofautiana na Mkapa Mkapa akiuka sera yake-Chuo Kikuu Uandikishaji wapiga kura waanza CUF yataja wagombea wake Temeke CCM yamtuhumu Mwenyekiti wake pandikizi Propaganda ya Udini itaisambaratisha nchi - CHADEMA USHAURI NASAHA
MAKALA
MIPASHO NASAHA
MAKALA
KALAMU YA MWANDISHI
Je, unajua haki yako unapokamatwa na polisi? LISHE
|
|
|
|
|