AN-NUUR 
Na.178 Shaaban  1419, Desemba 4 - 10, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
MASHAIRI:
 

NYERERE  UMESAHAU?! 

1. Kumradhi Mhariri, niweke japo pembeni, 
    Dosa Aziz Mahiri, Rama Mashando Plantani, 
    Dustan wa Omari, Takadir, Selemani, 
 Nyerere umesahau, mashujaa wa uhuru. 

2. Wajukuu taabani, Nyerere umesahau, 
    Islam Gerezani, utadhani maumau, 
    Chuki mwana Athumani, Mola ammpe nafuu, 
 Nyerere umesahau, mashujaa wa uhuru. 

3. Abduwahad Saki, uhuru kapigania, 
    Tena naye Ally Saki, John Rupia shawia, 
    Ni vipi hawazinduki, hao ulowaacha, 
 Nyerere umesahau, mashujaa wa uhuru. 

4. Pat mwana wa Kunambi, Tabora Bantu Kasela, 
    Wapeleka rambirambi, wakirejea kwa Mola, 
    Uhaiwao vitimbi, sasa twafia jela, 
 Nyerere umesahau, mashujaa wa uhuru. 

5. Kumsahua Milinga, Germa Pacha Kimalando, 
    L. MwanaMakaranga, Nusura yake upondo, 
    Asha Ngoma mwana Yanga, jina lake ni mdondo, 
 Nyerere umesahau, mashujaa wa uhuru. 

6. Japhet mwana Kirilo, Saadani Abdi Kandoro, 
     Bugohe Kitwana Kwalo, jina lenye mgogoro, 
    Titi Mohammed Kolo, Iddi mwafongo Kasoro, 
 Nyerere umesahau, mashujaa wa uhuru. 

7. Mohammed Mtamila, na Tatu Bonyi Mzee, 
    Haidari Mwinyimvua, Saidi Tanu Tawae, 
    Gerezani wanalia, Islamu uwatoe, 
 Nyerere umesahau, mashujaa wa uhuru. 

8. Ramia Mwana Hamadi, naye Hassani Amiri, 
    Ulichukuwa ahadi, Islam kustiri, 
    Walsh Alikurudi, Dosa kabeba Khatari, 
 Nyerere umesahau, mashujaa wa uhuru. 

Masare S.R. Ndwata (Mrambowa ’71), 
S.L.P. 70535, 
Dar es Salaam. 



Uhodari gani huo wa majumba kuchomwa moto? 

1. Gari limepamba moto, Abiria sote mbio, 
    Na dereva Kiroboto, mtu asomasikio, 
    Hata panapo mkito, mwendo wake yeye mbio, 
 Uhodari gani huo, majumba kuchomwa moto? 

2.  Cheo chanzo cha mapato, siwatu kosa mafao, 
    Leo wakubwa watoto, hawahishiwi kilio, 
     Bado wapo tumbo joto, kwa kusoka kwa makao, 
Uhodari gani huo, majumba kuchomwa moto? 

3. Kuchomewa nyumba moto, hali kuwafikirio, 
   Awamu hii majuto, zimekithiri tukio, 
   Uwamuzi wa mkato, mwavuruga vyenu vyeo, 
Uhodari gani huo, majumbe kuchomwa moto? 

4. Nyoyo zenu sitakato, mwathamini oshanguo, 
    Na mlalapo kwa mito, mwaoga kwa misuguo, 
    Fadhira zenu mpito, hamkumbuki chaguo, 
Uhodari gani huo, majumbe kuchomwa moto? 

5. Kutokuwa hata ndoto, katika lile tukio, 
    Mlihuwa na watoto, ma kaka na baba zao, 
    Mwaka hujawa mpito, Wanzasa nao vilio, 
Uhodari gani huo, majumba kuchomwa moto? 

6. Mwembe Chai, swala zito, lipi kwenu listuo, 
    Asikali kila pato, na wakuu wa vituo, 
    Kuja leta mkong’oto, hati hudai tishio, 
Uhodari gani huo, majumba kuchomwa moto? 

7. Njia nikua mpito, Wallahi kwa siku hiyo, 
    wenyewe bila msito, kwa kuvaa kwao ngao, 
    Asikali wa mseto, Polisi fefu yu nao, 
Uhodari gani huo, Majumba kuchomwa moto? 

9. Beti nafanya mkato, Sitozidi endeleo, 
    Sikulia si kushoto, nafanya maangalio, 
    Nafananisha na chato, alapo pasi mlio, 
Uhodari gani huo, Majumba kuchomwa moto? 

Dk. Shamte “A’ Mpita (Kijukuu cha Malenga), 
c/o Lambalamba, 
S.L.P. 66563, 
Dar es Salaam. 


Watatu kuwa mmoja 

Ongeza moja na moja, mbili jibu utapata, 
Kizidi nyingine moja, huwa tatu siyo sita, 
Kusema jibu ni moja, unayaleta matata, 
 Hesabu sijaiona, watatu kuwa mmoja. 

Ya hivyo sikuiona, shule zote nilopita, 
Yeyote ataiguna, kwa kuona ina tata, 
Jaribu kutwa mchana, jawabu kulitafuta, 
 Hesabu sijaiona, watatu kuwa mmoja. 

Baba na mwana pamoja, na roho akiwakuta, 
Ni watatu bila hoja, akilini inakita, 
Vingine huwa kioja, bure tabu mnaleta, 
 Hesabu sijaiona, watatu kuwa mmoja. 

Kauli hii kunena, hakika inawasuta, 
Mashiko hasa haina, kwenye hoja kuileta, 
“Mtafuma na kushona”, kinyume hamtopata, 
 Hesabu sijaiona, watatu kuwa mmoja. 

“Baba” huyo ni mmoja, hesabu inavyoleta, 
:”Mwana” kwa Baba akija, wawili tunawapata, 
Jaribu vyanda kukunja, jawabu linajileta, 
 Hesabu sijaiona, watatu kuwa mmoja. 

“Fumbo”tumeshaliona, twaliachia kupita, 
Nasi huko kubishana, twakatazwa katakata, 
Tunayo bora hazina, mafunzo yalotakata, 
 Hesabu sijaiona, watatu kuwa mmoja. 

Witiri Mungu mmoja, uungu hana mwambata, 
Pekee ninamtaja, mwenziwe hutompata, 
Nufusi tatu kutaja, moyo wangu unasita, 
 Hesabu sijaiona, watatu kuwa mmoja. 

JIHAD R. SABALLA, 
S.L.P. 347, SHINYNAGA. 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
'White Paper  ni ulaghai wa  Serikali ya CCM' 
Na Mwandishi wetu 

Sheikh Omar Bashir awekwa rumande 
Na Mwandishi Wetu 

Mpango wa 'Kupindua' uongozi wa  Bakwata: Masheikh Dar waitwa polisi kuhojiwa 
Na Mwandishi Wetu 

Zahrau Day yatikisa Tanga 
Na Mwandishi Wetu 

MAKALA: Hatuna haja ya maelekezo ya yule aliyetufikisha hapa  
Na Alhaj Yusuf Kalala, Washington DC USA 

Huduma za afya Kondoa haziridhishi 
Na Abu Zubeir 

Wasemavyo wanaharakati 

Tunahitaji 'UN' ya Waislamu! 
Na Twahir Rashid 

Hoja binafsi: Wawekezaji watuondokesha makwetu 

Jamii inapokuwa soko huria...  
Na Said Rajab 

Someni kwa ajili ya Allah - Sheikh Baruti  
Na Muhibu Said 

Madrasa Al-Ii'Tiswamu Al-Umaahaati Fiisabiililillah - Moro 
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Madrasat Hidayat Mbagala 
Na Mussa Salum  

Hali ya Uislamu Moro Vijijini yazidi kuwa mbaya  
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Sheikh Masoud Mwinyi awaonya Waislamu kuacha migogoro Babati  
Na Abu Zuberi - Babati 

Tusikaribishe mfungo wa Ramadhani kwa Vunja Jungu  
Na Abeid Poyo 

'Acheni zinaa muepukane na ukimwi'  
Na Mussa Salum 

Wavunja jungu watahadharishwa 
Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

Hoja/Uchambuzi: 
Je, hivi tuendelee kushika amri za Mungu tena? 
Na Mwinjilisti Bunga E. Dettu 

Njia ya uzimani ni nyembamba,  waionao ni wachache 
Na Yasin Valerian Massawe 

Habari: 
Semina ya Maimamu Tanga yadai: Maimamu wanapuuzwa  
Na Mwandishi Wetu 

Kesi ya Waislamu Mwembechai yaahirishwa kwa mara nyingine  
Na Muhibu Saidi 

Kongomano la wanawake wa Kiislamu Bagamoyo 
Na Mwandishi Wetu 

Sayansi na Teknolojia 
[Kuongeza RAM kwenye Kompyuta] 
 
Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Madini ya Zinc] 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita