|
|
|
• Watakiwa kuwa na kauli moja • Waonywa wasing’ang’anie
Uimamu
Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kwamba hadhi na thamani ya Maimamu nchini imekuwa ya chini sana kiasi kwamba hata waumini wenyewe wamefikia hatua ya kuwapuuza. Aidha kutokana na Maimamu kutokuthaminiwa na nafasi zao kama viongozi wa Waislamu kutokutambuliwa katika jamii, malalamiko ya Waislamu yamekuwa hayasikilizwi wala kupewa umuhimu wowote. Wakizungumza katika semina ya Maimamu iliyoandaliwa na Taasisi ya Jamaatul Kheir, baadhi ya Maimamu pamoja na kuonyesha dosari hiyo kubwa wamesema kwamba imekuwa ni vigumu kilio cha Waislamu kusikilizwa kwani Maimamu wenyewe hawana kauli moja. Sheikh Mohammed Idd katika nasaha zake, alisema kwamba ni muhimu Maimamu waungane wawe kitu kimoja ili kuziba mwanya ambao maadui waweza kuutumia kuwaparaganya Waislamu. Akizungumza katika semina hiyo iliyofanyika Novemba 29, mwaka huu katika hoteli ya Kola Prieto, Sheikh Abdallah Bawaziri aliwahimiza Maimamu wawe wanakutana mara kwa mara kusalimiana na kujuliana hali kama njia moja ya kufikia kwenye umoja alioutaja Allah (s.w.) katika Qur’an (3:103). Naye Sheikh Mohammed Kombora aliwatanabahisha Maimamu wasiwe ni wenye kung’ang’ania Uimamu pale waumini wanaponyesha kutokuridhika na utendaji wao. Kwa upande mwingine Sheikh Kombora aliwakumbusha Waislamu kuwa wanawajibika kumtii Imamu na kama Imam huyo kakiuka maadili basi juhudi za mara moja zifanywe kumuweka mwingine. Semina hiyo ya Maimamu imekuwa ni ya kwanza na ya pekee mjini Tanga kwani imewakutanisha Maimamu kutoka zaidi ya Misikiti 40 iliyo chini ya taasisi mbalimbali. Sheikh Ali Zumo kutoka Ansaar Suna ndiye aliyesoma Qur’an tukufu ya ufunguzi ambayo ilifasiriwa na Sheikh Suleiman Bakar wa TAMTA. Sheikh Suleiman katika kuifasiri aya ya 35 ya Suratul-Nuur aliwataka Waislamu wawe ni nuru ya kuongoza umma katika kheri. Katika hotuba ya kuwakaribisha wanasemina, Sheikh Shauri Abubakar wa Jamaatul Kheir alizitaka taasisi mbalimbali za Kiislamu kujiimarisha na kusambaza huduma zao hadi ngazi za wilaya na kata. Katika jumla ya maazimio ya semina hiyo ni kwamba fursa ziandaliwe ili
Maimamu wawe wanakutana mara kwa mara ili kujenga umoja na uongozi imara
wa Waislamu.
• Yadaiwa hakimu anaumwa • Kesi nyingine
kusikilizwa Kisutu
Na Muhibu Saidi KESI ya tuhuma ya kufanya "ghasia" maeneo ya Mwembechai, Jijini Dar es Salaam iliyofunguliwa na serikali katika mahakama ya Kivukoni, Jijini dhidi ya Waislamu kumi imeahirishwa tena hadi Desemba 21, mwaka huu, tarehe ambayo inatazamiwa tena kuanza kusikilizwa. Kesi hiyo ilipangwa kuanza kusikilizwa mahakani hapo mapema Desemba 2, mwaka huu, ambapo mashahidi wa upande wa serikali walitarajiwa kutoa ushahidi wao. Hata hivyo, mahakama hiyo imeamua kuahirisha kesi hiyo kwa madai kwamba Hakimu anayesikiliza kesi hiyo Bw. Gabriel Mirumbe anaumwa. Kesi hiyo yenye namba 407/98 ilifunguliwa mahakama ya Hakimu mkazi ya Kisutu, Jijini mapema mwezi Machi , mwaka huu ambapo baadae ilihamishiwa katika mahakama ya Kivukoni Jijini Dar es Salam, Watuhumiwa katika kesi hiyo ni pamoja na Rutemba Shaaban, Iddi Selemani, Ismaili Hamisi, Jafari Mohamed, Omari Hemed, Hassan Habibu, Hamisi Nassoro, Ally Daudi, Juma Ali na Nurdin Abbas. Wakati huo huo, kesi nyingine namba 184/98 ya tuhuma ya kufanya ghasia na kujeruhi inayowakabili Waislamu kumi na mmoja, inatazamiwa kuanza kusikilizwa hapo Desemba 14, mwaka huu katika mahakama ya Kisutu, Jijini Dar es Salaam. Aidha, kesi nyingine namba 192/98 ya tuhuma ya kufanya ghasia, kuharibu
mali hapo Mwembechai, inayowakabili Waislamu wengine kumi na mbili nayo
pia inatazamiwa kuendelea kusikilizwa hapo Desemba 14, mwaka huu pia katika
mahakama ya Kisutu.
Kikwete, Msabaha, Mikidadi, Ramiya, Kimbau kualikwa Na Mwandishi Wetu Kongamano la wanawake wa Kiislamu litakalofanyika mjini Bagamoyo hivi karibuni linatazamiwa kuhudhuriwa na maelfu ya wanawake kutoka sehemu mbali mbali nchini. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Wanawake wa Kiislamu nchini, Bi Fatma Lazaro kongamano hilo litawashirikisha wanawake kutoka mikoa ya Pwani, Dar es Salaam, Morogoro, Iringa na Dodoma. Mwenyekiti huyo amesema huenda wakawalika Wabunge wa Mkoa wa Pwani katika kongamano hilo. "Tutawaalika waheshimiwa Waheshimiwa Jakaya Kikwete, Dk. Msabaha, Prof.
Mikidadi, Ramiya na Kanali Kimbau katika kongamano ili tuwakabidhi risala
na maazimio yetu" alisema Mwenyekiti huyo, alipokuwa akizungumza na mwandishi
nyumbani kwake Manzese Jijini Dar es Salaam.
|
YALIYOMO
'White Paper ni ulaghai wa Serikali ya CCM' Na Mwandishi wetu Sheikh Omar Bashir awekwa rumande
Mpango wa 'Kupindua' uongozi
wa Bakwata: Masheikh Dar waitwa polisi kuhojiwa
Zahrau Day yatikisa Tanga
MAKALA: Hatuna haja ya maelekezo ya
yule aliyetufikisha hapa
Huduma za afya Kondoa haziridhishi
Tunahitaji 'UN' ya Waislamu!
Hoja binafsi: Wawekezaji watuondokesha makwetu Jamii inapokuwa soko huria...
Someni kwa ajili ya Allah - Sheikh
Baruti
Madrasa Al-Ii'Tiswamu
Al-Umaahaati Fiisabiililillah - Moro
Madrasat Hidayat Mbagala
Hali ya Uislamu Moro
Vijijini yazidi kuwa mbaya
Sheikh Masoud Mwinyi awaonya
Waislamu kuacha migogoro Babati
Tusikaribishe mfungo wa Ramadhani
kwa Vunja Jungu
'Acheni zinaa muepukane
na ukimwi'
Wavunja jungu watahadharishwa
Hoja/Uchambuzi:
Njia ya uzimani ni nyembamba,
waionao ni wachache
Habari:
Kesi ya Waislamu Mwembechai
yaahirishwa kwa mara nyingine
Kongomano la wanawake wa
Kiislamu Bagamoyo
Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|