AN-NUUR 
Na.178 Shaaban  1419, Desemba 4 - 10, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Hali ya Uislamu Moro Vijijini yazidi kuwa mbaya
 

• Kiwege kijiji chenye Waislamu wengi hakina msikiti 

• Makanisa yajengwa na kubatiza Waislam 

• Hutembea kilometa 10 kuswali Ijumaa 
 

Na Rajab Rajab, Morogoro 
 

HALI ya Uislamu katika vijiji vingi vyenye Waislamu wengi Mkoani hapa ipo mashakani kufuatia vijiji hivyo kukosa misikiti, madrasa pamoja na masheikh na kufikisha ujumbe, hali iliyopelekea makanisa kuvamia vijiji hivyo na kuwabatiza mamia ya Waislamu. 

Uchunguzi uliofanywa na Mwandishi wa habari hizi katika Tarafa ya Ngerengere hususan katika kijiji cha Kiwege umebaini kuwa tangu tupate uhuru mwaka 1961 kijiji hicho kilikuwa na asilimia 95 ya Waislamu wanaoishi kijijini hapo, lakini wengi wao hivi sasa wamebatizwa. 

Kadri miaka ilivyozidi kusogea ndivyo Uislamu katika kijiji hicho ukawa unapotea hasa kutokana na kukosekana msikiti pamoja na madrasa, jambo ambalo lilipelekea dini nyingine kuingia kijijini hapo kwa kasi na kuwabatiza Waislamu ambao wengi wanaona bora waingie katika dini hiyo kuliko kuwa Waislamu bila ya kuufahamu Uislamu wenyewe. 

Baada ya hali ya Uislamu kuendelea kuwa mbaya kijijini hapo, kukatokea vijana wenye uchungu na dini yao ambapo mnamo tarehe 24, June, 1998 kuanzisha madrasa chini ya Mwembe kwa lengo la kuwafundisha watoto wadogo kwa matazamio ya kuja kunusuru Uislamu kijijini hapo. 

Madrasa hiyo iliyopewa jina la Rukhuman la kijiji Kiwege kilometa 10 kutoka Ngerengere ulianzishwa na Ustaadh Yusufu Ally Mohamed, Saidi Ally Mbulu pamoja na Juma Rashid Mlali ambapo wawili kati yao wanakaa mjini Morogoro na wanalazimika karibu kila siku kufanya safari ya kwenda kufundisha madrasa hiyo ambayo ina wanafunzi 103 wasichana kwa wavulana. 

Akiongea na gazeti hili mmoja na walimu hao amesema kama kuwa kijiji chao hakina msikiti wao na baadhi ya Waislamu wengine wanalazimika kila Ijumaa kusafiri kwa mguu mwendo wa kilomekta kumi (10) kutoka kijijini kwao Kiwege mpaka Ngerengere kuswali Ijumaa, huku wakiwaacha Waislamu wenye imani ndogo, wagonjwa na wanawake nyumbani. 

Katika kujikwamua na hali ya kukosa msikiti waalimu hao kwa kushirikiana na wanafunzi na madrasa na baadhi ya Waislamu wa kijiji hicho wameanza kuzungushia miti katika eneo la madrasa ambapo wanajaribu kuziba zulia ili wapate sehemu ya kufanyia Ibada. 

Mbali ya Madrasa hiyo iliyoanzishwa chini ya Mwembe, na kuwa kero wakati wa mvua na jua, pia madrasa hiyo iliyotembelewa na mwandishi wa habari hizi ina upungufu wa majamvi ya kukalia na majuzuu ambapo wastani na juzuu moja linasomwa na watoto kumi kwa wakati mmoja hali ambayo ni kinyume kabisa na taratibu za ufundishaji. 

Walimu hao wa madrasa wamewaomba Waislamu popote pale walipo katoa misaada yao kwa ajili ya kuunusuru Uislamu kwa kujenga msikiti na madrasa ambapo wanakijiji wa Kiwege nguvu zao ni ndogo na ukizingatia kijiji hicho sasa hivi kimekumbana na njaa. 


Sheikh Masoud Mwinyi awaonya Waislamu kuacha migogoro Babati
 

Na Abu Zuberi - Babati 
 

IMAM wa Msikiti Mkuu wa Ijumaa Mjini Babati, Sheikh Masoud Mwinyi amewatahadharisha Waislamu kuacha migogoro, kwa kuwaambia kamba penye migogoro kamwe hapawezi kukapatikana maendeleo. 

Sheikh Mwinyi aliyasema hayo katika madrasa yake alipotembelewa na ugeni uliotoka mjini Dodoma, ugeni huo uliongozwa na Sheikh Abdallah Ally wa Masjid Qubaa, Bwana Khalifa Abdallah (Hongera) na Ustadh Idrisa Simba. 

Sheikh Mwinyi alisema migogoro iliyodumu kwa muda hapa nchini hasa ile ya Misikiti imesababisha waumini kutokuwa na msimamo wa kushirikiana na viongozi wao kuleta maendeleo katika sehemu zao. 

"Muda mwingi unatumika pamoja na fedha kwa ajili ya kuweka mawakili kutatua kesi za kugombania Msikiti, inafikia hata mahakama kuyarudisha masuala hayo katika mikono ya Waislamu, Misikiti yote ni ya Mwenyezi Mungu iwe inamilikiwa na Taasisi au mtu binafsi au kikundi fulani, hiyo yote ni Misikiti ya Allah (s.w.) iheshimiwe na kuwaacha Waislamu waitumie katika kumwabudu Allah (s.w.)", alisema Sheikh Msoud. 

Alishauri kwamba Taasisi kubwa za Kiislamu zikae na kuona ni wakati muafaka kuhamasisha maendeleo kwa waumini wao. 

"Waislamu wanahitaji mambo mengi, vituo vya elimu, vituo vya kulea watoto yatima, miradi ya uchumi, uimarishaji wa Da’awah, mambo haya yatapatikana tu pale migogoro itakapotatuliwa na kuachwa mara moja", alisisitiza Sheikh Masoud. 

Aidha Sheikh Masoud alisema wanafunzi wake hulipa umuhimu suala la elimu, na nidhamu yake pia kwani bila ya nidhamu elimu haitapatikana. 

Akiunga mkono wito huo, Sheikh Abdallah Ally alisema, migogoro ya Misikiti ingeweza tu kupatikana ufumbuzi na Waislamu wenyewe bila ya hata kupoteza fedha na muda kwenda mahakamani. 

Sheikh Masoud anaendesha Da’awah kwa kuwa na madrasa za watoto, na hata watu wazima. Kwa hivi sasa ameanza ujenzi wa jengo jipya la Msikiti ambalo kwa sasa linahitaji msaada wa nondo, saruji na kokoto kwa mujibu wa tangazo lililopo Msikitini karibu na Madrasati Al-Hijira. 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
'White Paper  ni ulaghai wa  Serikali ya CCM' 
Na Mwandishi wetu 

Sheikh Omar Bashir awekwa rumande 
Na Mwandishi Wetu 

Mpango wa 'Kupindua' uongozi wa  Bakwata: Masheikh Dar waitwa polisi kuhojiwa 
Na Mwandishi Wetu 

Zahrau Day yatikisa Tanga 
Na Mwandishi Wetu 

MAKALA: Hatuna haja ya maelekezo ya yule aliyetufikisha hapa  
Na Alhaj Yusuf Kalala, Washington DC USA 

Huduma za afya Kondoa haziridhishi 
Na Abu Zubeir 

Wasemavyo wanaharakati 

Tunahitaji 'UN' ya Waislamu! 
Na Twahir Rashid 

Hoja binafsi: Wawekezaji watuondokesha makwetu 

Jamii inapokuwa soko huria...  
Na Said Rajab 

Someni kwa ajili ya Allah - Sheikh Baruti  
Na Muhibu Said 

Madrasa Al-Ii'Tiswamu Al-Umaahaati Fiisabiililillah - Moro 
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Madrasat Hidayat Mbagala 
Na Mussa Salum  

Hali ya Uislamu Moro Vijijini yazidi kuwa mbaya  
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Sheikh Masoud Mwinyi awaonya Waislamu kuacha migogoro Babati  
Na Abu Zuberi - Babati 

Tusikaribishe mfungo wa Ramadhani kwa Vunja Jungu  
Na Abeid Poyo 

'Acheni zinaa muepukane na ukimwi'  
Na Mussa Salum 

Wavunja jungu watahadharishwa 
Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

Hoja/Uchambuzi: 
Je, hivi tuendelee kushika amri za Mungu tena? 
Na Mwinjilisti Bunga E. Dettu 

Njia ya uzimani ni nyembamba,  waionao ni wachache 
Na Yasin Valerian Massawe 

Habari: 
Semina ya Maimamu Tanga yadai: Maimamu wanapuuzwa  
Na Mwandishi Wetu 

Kesi ya Waislamu Mwembechai yaahirishwa kwa mara nyingine  
Na Muhibu Saidi 

Kongomano la wanawake wa Kiislamu Bagamoyo 
Na Mwandishi Wetu 

Sayansi na Teknolojia 
[Kuongeza RAM kwenye Kompyuta] 
 
Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Madini ya Zinc] 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita