AN-NUUR 
Na.176 Shaaban  1419, Novemba 20 - 26, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Sakata la mabucha ya Nguruwe kuibuka upya: 

Waislamu watoa onyo la mwisho 

Serikali nayo yachukua tahadhari 

Na Mwandishi Wetu

WAISLAMU na wananchi waishio Mwembe Madafu kata ya Ukonga wametishia kuchukua hatua mkononi endapo malalamiko yao dhidi ya uchomaji mishikaki katika maeneo yao hayatasikilizwa na vyombo vya dola. 

Wakiongea na gazeti hili, wananchi hao wamedai kwamba pamekuwa na uuzaji holela na uchomaji nyama ya nguruwe bila ya kuzingatia imani na hisia za wengine. 

Taarifa ya wajumbe saba wa mashina ya kata hiyo imedai kwamba Chaki amekuwa akiuza nyama ya nguruwe pamoja na mishikaki yake karibu na eneo la Msikiti. 

Aidha, wamesema kwamba hapo hapo anapouzia nyama ya nguruwe huuzwa pia Chips ambazo hununuliwa na watu mbalimbali wapita njia. 

Wajumbe hao Selemani Baridi, Mmasi Jihad Komba, Hassan Muhenga, Abdallah Hassan na Venant Baridi wameitahadharisha serikali ya mtaa ilifikishe suala hilo ngazi za juu na hatua za haraka zichukuliwe kabla ya kutokea matatizo. 

Katika kufuatilia suala hilo, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa - Mwembe Madafu Bw. T.F. Komba amemuamuru Bw. Chaki kuacha mara moja uchomaji huo wa nyama ya nguruwe katika eneo hilo. 

Katika barua yake ya Novemba 13, ameeleza kwamba mazingira anayochomea nyama hiyo ya nguruwe hayafanani na biashara hiyo na zaidi hata leseni hana. 

Aidha, barua hiyo imesema kwamba kwa kuwepo karibu na Msikiti na kuchanganya chips, kuku na nguruwe ni kukaribisha matatizo ya kuharibu amani na usalama wa raia. 

Ni kwa sababu hiyo barua ya serikali ya Mtaa imemalizia kwa kumwambia Bw. Chaki "Unaamriwa ... acha mara moja kuchoma nyama ya nguruwe, vinginevyo hatua kali dhidi yako zitachukuliwa". Hata hivyo, barua hiyo haikufafanua ni hatua zipi zingechukuliwa. 

Sakata ya uvunjaji wa bucha za nguruwe Jijini Dar es Salaam mwaka 1993 ilitokea baada ya malalamiko ya maimamu wa Misikiti kupuuzwa na serikali. Upuuzaji huo uliwapelekea waathirika kuchukua sheria mkononi. 

Kutoka uvunjaji wa bucha sakata hiyo ilichukua sura mpya na kufanywa operesheni maalum dhidi ya Waislamu walioitwa wa siasa kali. 

Operesheni hiyo iliharibu mahusiano kati ya Waislamu na serikali yao na zaidi kati ya Waislamu na Chama Cha Mapinduzi. 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
Maoni 
Kuwa na mawazo ya kufugwa tunajidharaulisha 

Sakata la mabucha  ya Nguruwe kuibuka upya 
Na Mwandishi Wetu  

Kondom sio kinga ya Ukimwi 

Bakwata yairushia polisi makombora Ngaramtoni 

MACHO YA SHUTUMA 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Serikali yatakiwa iwachukulie hatua wauaji 
Na Mwandishi Wetu 

Historia ya Msikiti wa Ngaramtoni 

Silaha yetu ni kura ya pamoja 
Na Alhaj Yusuf Kalala, Washington DC  U.S.A 

Anuani ya fikra 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Kuukaribisha mwezi mtukufu 

Tunahitaji "UN' ya Waislamu! 
Na Said  Rajab 

Kongamano la wanawake wa Kiislamu Newala lafana 

Umuhimu wa Elimu ya Awali kwa watoto wadogo - 2 
Na Ustaadh Kupa Pazi Said 

Kesi mojawapo ya mihadhara yafutwa 

Wasaidieni watoto wenye vipaji - Prof. Kilonzo 

Mahafali ya kidato cha nne Thaqafa: Wazazi wakumbushwa wajibu wao 

Wanafunzi Mwanza wadai haki za kuabudu mashuleni kwa usawa 
Na Iddi M. Katiba, Mwanza 

Saidianeni katika shida - Sheikh Abdallah 

Waislamu, Wakristo Rufiji watakiwa kuunda umoja 

Someni  muiokoe jamii kimaadili 

Acheni Shirki 

Kesi nyingine ya Waislamu Mwembechai yaahirishwa 
Na Muhibu Said 

Kusilimu kwa Wakristo kwaleta kero Mwanza 

Nzasa waomba msaada wa chakula, madawa 

Katibu wa Bakwata Moro ang'olewa Msikitini 

Masomo ya Dini ya Kiislamu  

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Umuhimu wa chakula katika shule za awali]  

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita