AN-NUUR
Na.165 Jamadul Awwal 1419, Septembe 4 - 10, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Dhana ya Udugu wa kiislamu 

Mafungamano ya Imani katika Uislamu yana haki, thamani na uzito zaidi kuliko udugu wa damu, nasaba,ukoo, kabila, Taifa au udugu wa aina nyingine yoyote ile: 

Hakika waumini wote ni ndugu" (49:10). 

Uzito wa mafungamano hayo ya kiimani umezingatia udugu wa Wanaadamu wote kwamba wanatokana na baba na mama mmoja, yaani asili moja na wote wanaiwania hatima moja. 

Umoja na udugu wa binaadamu unatokana na hao binadamu kuwa ni kizazi cha Adamu na Hawa. Kila binadamu ni memba wa familia hii, na hivyo kila memba anastahiki kupata haki zake katika familia hii kama alivyopia na dhima ya kutimiza wajibu wake. 

Udugu wa kiimani haukomei katika kuwa na asili moja bali pia katika kuwa na lengo na nafasi moja hapa ulimwenguni, Mwenyezi Mungu anatufahamisha katika Qur’an: (7:172), (49:13). 

Upeo huu mpana wa Qur’an kuhusu asili ya mwanaadamu, ndiyo kiini cha udugu mzito wa kiimani katika Uislamu. 

Udugu huo unaimarika zaidi ndani ya makundi ya harakati za Kiislamu yenye madhumuni ya kufanya mageuzi ya Kiislamu katika jamii. Mageuzi ambayo si tu yatasimamisha haki bali pia yatajenga na kuboresha utu, mahusiano na maaingiliano ya wanajamii chini ya mfumo mpya wa sera na itikadi inayokwenda sambamba na maadili yake, yaliyofunzwa na kudhibitiwa na mjuzi, makamilifu na Muumba wa vyote. Kujenga udugu na mafungamano haya ya kiimani kwahitajia mazoezi ya muda mrefu yenye kuandamana na hatua mbali mbali za utekelezaji na ufuatiliaji. 

Kuhusu msisitizo wa udugu wa kiimani katika kujizatiti kuondoa dhulma Qur’an yatueleza: 

Enyi mlioamini shikeni hadhari zenu, tokeni(kwenda vitani) mmoja mmoja au kwa pamoja. (4:71) 

Na mna nini hampigani katika njia ya Mwenyezi Mungu na (katika kuwaokoa) wale walio dhaifu katika wanaume na wanawake na watoto ambao husema Mola wetu! tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhalimu na utujaalie tuwe na ulinzi unaotoka kwako na tujaalie tuwe na kutunusuru anaetoka kwako" (4:7). 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 
 
TAHARIRI 
HAKI YA KUABUDU MASHULENI: Hoja ya uwingi isizuie haki ya wachache 

Aliyeandika Yesu si Mungu bado akabiliwa na kesi 
Na Mwandishi Wetu 

Wazazi walia na Mkuu wa shule Mkwawa 
Na Mwandishi Wetu, Iringa 

Serikali iache kudhulumu  Waislamu - Bakwata  
Na Mwandishi Wetu

KESI YA MIRATHI: Hukumu ya Jaji Agostino yatupwa 
Na Mwandishi Wetu 

Sumaye sasa atoa ‘waadhi’ Msikitini 
Na Mwandishi Wetu, Arusha 

Sekondari ya Kiislamu Sumbawanga, mtihani kwenu – Sheikh Akilimali 
Na Harun Rashid, Sumbawanga 

37 wasilimu  Mwanza 
Na Mwandishi Wetu, Mwanza 

Akamatwa kwa kusoma gazeti la ANNUUR ! 

MGOGORO WA CHWAKA NA MARUMBI: Serikali ya Dk. Salmin itafute ufumbuzi 
Na Mwandishi Wetu, Pemba 

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 4 

Kwa nini walengwa wa mabomu wawe ni Marekani? 
Na Maalim Ali Bassaleh 

Profesa amekosea kusema kwamba... 
Na A.M. Hamza 

Ugaidi ni ugaidi, hata wa Marekani ni ugaidi 
Na Maalim Ali Bassaleh 

Dhana ya Udugu wa kiislamu 

UGAIDI: Chanzo si magaidi, ni dhuluma ya Marekani 
Na HASSAN KIMANGALE 

Jengeni familia bora 
Na Abuu Said, Iringa 

Tuwasaidie Waislamu kielimu na kiuchumi - Bi Zuhura 
Na SAID RAMADHANI KISSIMBA 

Tumieni uhuru wenu vyema 
Na Abuu Zaina, Iringa 

Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu,  ni uzushi mtupu! - 4  
Na Muhibu Said 

Mihadhara ya Wakristo yatawala Handeni 
Na Mwandishi Wetu, Handeni 

Ziara ya Kadinali Pengo Moro  
Na Mussa Ally, Morogoro 

Aonyesha ujuzi wa kutengeneza Trekta 
Na Mwandishi Wetu 

Waislamu wasizifanye sharia za dini kuwa nzito – Sheikh Mzonge 
Na Ashraf  Yusuf, Moshi 

Sengerema waomba msaada 
Na Idd Katimba, Mwanza 
 
Mafundisho ya Quran 

Barua za wasomaji 

Mashairi: 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Matunzo ya mtoto mwenye lishe duni 

Matangazo 
 
 

 

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita