|
|
| Hoja
za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu, ni uzushi mtupu! - 4
Na Muhibu Said Kuhusu huyo Roho Mtakatifu aliyetabiriwa na Yesu bado ni Nabii Muhammad (s.a.w) kwa kuwa lipo sharti moja muhimu alilolitaja Bwana Yesu la kuondoka kwanza yeye (Yesu) ndipo huyo msaidizi mwingine aje. Na Mtume Muhammad (s.a.w) alitumwa na Mwenyezi Mungu (s.w.t) pamoja na mambo mengine alikuja kutangaza kwamba ndiye Nabii aliyebashiriwa kuja kwa Nabii Isa au Yesu (a.s.). Yesu alisema: "Lakini mimi nawaambia iliyokweli, yawafaa ninyi mimi niondoke kwa maana mimi nisipoondoka, huyo msaidizi hatakuja kwenu, bali mimi nikienda zangu nitampeleka kwenu". (Yohana 16:7). Kauli hiyo ya Yesu inatofautiana wazi na dai hilo la Bw. Augustine hasa tunaporejea katika maandiko mengine mengi ya Biblia yanayoonyesha kwamba Roho Mtakatifu wanayemfikiria Wakristo alikuwepo hata kabla Yesu hajazaliwa (Marko 12:36), kabla Yesu hajaondoka (Yohana 20:22-23), mama yake (Yesu) alichukua mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu (Luka 1:35) n.k. Kuhusu kudumu kwa huyo msaidizi kusudio lake siyo lazima Mtume Muhammad (s.a.w) awepo pamoja nasi kimwili. Lakini kudumu kwa usahihi kwa mafundisho yake ni hoja tosha ya kukiri kwamba Mtume Muhammad (s.a.w) yupo pamoja nasi daima. (Qur’an 2:154). Hii inafanana na ile kauli ya Yesu alipowaambia wafuasi wake kwamba: "…Natazama, mimi niko pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari. (Mathayo 28:20). Hii haina maana kuwa leo Yesu tuko pamoja naye duniani kimwili. Lakini watu walio duniani, lakini wakawa hawana faida wala manufaa yoyote kwa mwanadamu, watu kama hao ndio Bwana Yesu aliowaita kwamba ni "wafu" japokuwa wanapumua. (Mathayo 8:21). Kwa mantiki hiyo, ni dhahiri kuwa Yesu ndiye Isa aliyemtabiri Nabii Muhammad (s.a.w) kama nilivyoonyesha hapo juu kinyume na anavyopotosha Bw. Augustine. Bw. Augustine anaendelea kudai "Qur’an inasema Isa alitoa zaka (19:31). Katika Biblia hakuna sehemu yoyote ya aya inayosema Yesu alitoa zaka. Je, huoni kuwa nayo ni tofauti?" Mwisho wa kunukuu. Kama nilivyokwishabainisha hapo juu kwamba, Mwinjilisti Yohana amekwishaeleza kwamba "kuna mambo mengine mengi aliyoyafanya Yesu ambayo hayakuandikwa kwa kuhofia vitabu vingekuwa vingi sana duniani (Yohana 20:25). Kwa hiyo, jambo la Bwana Yesu kutoa zaka ni katika orodha ya mambo hayo ambayo hayakuandikwa katika Biblia. Na ndio maana Qur’an Tukufu ikalazimika kukumbusha kwamba "Nabii Isa au Yesu" aliusiwa na Mola wake kutoa zaka. (19:31) Haijulikani jambo zito na muhimu kama hilo lisizungumzwe na Biblia hasa ukizingatia kwamba Bwana ndiye mfano mwema kwa wafuasi wake katika kila fundisho la Mwenyezi Mungu! (Yohana 14:6). Kwa mantiki hiyo, dai hilo la Bw. Augustine bado halijamtofautisha Yesu na Isa mpaka tuyapate mambo yote aliyoyafanya Yesu. Bw. Augustine anaendelea kusema "Biblia inasema Yesu alisulubiwa na kufa msalabani na hatimaye kufufuka" (Mathayo 16:21). Qur’an 4:157 inakataa kusulubiwa, kufa na kufufuka kwa Isa. Je, huoni huyo Isa na Yesu ni wawili tofauti? Mwisho wa kunukuu. Aya hiyo (ya Mathayo 16:21) ya Biblia aliyoitaja hapo juu Bw. Augustine inatia shaka kuamini kwamba ni Yesu ndiye aliyetamka maelezo yake, kwani naamini kwamba Yesu kamwee hawezi kutabiri jambo kisha lisitokee. Mwandishi wa aya hiyo Bwana Mathayo Mtakatifu anasema: "Tangu wakati huo Yesu alianza kuonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa Makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka" (Mathayo 16:20). Pamoja na maelezo hayo, lakini ukisoma Mathayo 27:27 unakuta waliompa mateso, kumsulubu mpaka kufa ni askari wala siyo wazee, wakuu wa makuhani wala waandishi kama ilivyotabiriwa na aya hiyo (ya Mathayo 16:21). Kwa utata huo, ndio maana Qur’an Tukufu ikathibitisha kwamba "Hawakumwua wala hawakumsulubu". (4:157-158). Na huu ni ushahidi tosha unaothibitisha kwamba Nabii Isa wa Qur’an ndiye Yesu wa Biblia. Isingekuwa hivyo, Qur’an isingejishughulisha kabisa na suala la kukanusha madai ya Wakristo ya kusulubiwa, kufa na kufufuka kwa Nabii Isa au Yesu (a.s.). Mwisho, Bw. Augustine anasema "Qur’an (10:94) inawaelekeza Waislamu wenye mashaka kama ndugu yangu Muhibu Said wawaulize watu wa vitabu wa kabla yao (Wakristo). Kwa kutojua maandiko watuulize nasi (Wakristo) tutawafundisha. Elimu ya kiroho wenzetu hawanayo (17:85). Mwisho wa kunukuu. Napenda kumuelewesha Bw. Augustine kwamba watu wa vitabu wa kabla yetu tulioagizwa tuwaulize siyo Wakristo na mtu kama Augustine anayezua na kupotosha wazi maandiko na ukweli kwa ujumla. Kwanza Wakristo ni watu waliozuka miaka mitatu baada ya Bwana Yesu (Nabii Isa) kuondoka (Matendo 11:25-26). Ni Uislamu na Waislamu wamekuwepo tangu zama za Nabii Adamu (a.s.) (30:30, 2:213). Hivyo, watu waliokuwa kabla yetu siyo Wakristo, bali ni Mayahudi na Manasara waliokuwa wakiijua kweli iliyokuwemo ndani ya Torati, Zaburi, Injili na Nyaraka sahihi za Manabii na kuifuata. Watu hao ni ndugu zetu Waislamu walitutangulia na siyo Wakristo. Aidha, elimu ya roho ambayo binadamu wote (na si Waislamu peke yao) ambayo hawakuwepwa isipokuwa kidogo, ni elimu ya kuijua kiundani roho ile inayompa uhai kiumbe, na si elimu ya "kiroho" kwa maana ya "ujuzi wa mambo ya Mwenyezi Mungu" kama anavyopotosha Bw. Augustine hapo juu. (Tafadhali asome tena mara kwa mara aya hiyo). Hakuna mtu yeyote anayeweza kuonyesha japo picha ya roho yake ilivyo. Namsihi Bw. Augustine kwamba mara nyingine asipende kuchanganya mambo kwa kuingiza mada isiyohusika katika mjadala husika. Kwa upande mwingine, kama alivyozua makusudi katika gazeti la Msemakweli
toleo la Juni 28 hadi Julai 4, 1998, kwamba Nabii Isa aliyemwita wa
Qur’an alifufua na kisha kuua, nampa Bw. Elia Batendi miaka miwili aonyeshe
aya hiyo ndani ya Qur’an Tukufu. Pia kama si uzushi wake, aonyeshe aya
katika Qur’an inayosema kwamba Bi. Mariamu alichukua mimba siku ile ile
na kumzaa Nabii Isa siku ile ile!
|
TAHARIRI HAKI YA KUABUDU MASHULENI: Hoja ya uwingi isizuie haki ya wachache Aliyeandika Yesu si Mungu bado akabiliwa
na kesi
Wazazi walia na Mkuu wa shule
Mkwawa
Serikali iache kudhulumu
Waislamu - Bakwata
KESI YA MIRATHI: Hukumu ya
Jaji Agostino yatupwa
Sumaye sasa atoa ‘waadhi’ Msikitini
Sekondari ya Kiislamu Sumbawanga,
mtihani kwenu – Sheikh Akilimali
37 wasilimu Mwanza
Akamatwa kwa kusoma gazeti la ANNUUR ! MGOGORO WA CHWAKA NA MARUMBI: Serikali
ya Dk. Salmin itafute ufumbuzi
MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 4 Kwa nini walengwa wa mabomu wawe ni
Marekani?
Profesa amekosea kusema kwamba...
Ugaidi ni ugaidi, hata wa Marekani
ni ugaidi
UGAIDI: Chanzo si magaidi, ni dhuluma
ya Marekani
Jengeni familia bora
Tuwasaidie Waislamu kielimu
na kiuchumi - Bi Zuhura
Tumieni uhuru wenu vyema
Hoja za kutofautisha Yesu na Issa
ni udhaifu, ni uzushi mtupu! - 4
Mihadhara ya Wakristo yatawala Handeni
Ziara ya Kadinali Pengo Moro
Aonyesha ujuzi wa kutengeneza
Trekta
Waislamu wasizifanye sharia
za dini kuwa nzito – Sheikh Mzonge
Sengerema waomba msaada
Chakula na Lishe
|