AN-NUUR
Na.157 Rabi' Awal 1419, Julai 10 - 16, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Ijue Madrastin-Nuur Ngaranaro 

Na Mwandishi Wetu, Arusha 

Madrasatin-Nuur iliyopo Ngaranaro Unga Limited ilianza takriban miaka 40 iliyopita; ilianzishwa na Mwalim Sultan kutoka Kondoa kama madrasa ya barazani. 

Mwalimu Saidi alichukua nafasi baada ya kifo cha Mwalimu sultan mwaka 1960 ikaongozwa na mwalimu Abdallah Saleh akifundisha Qur’an na Fiqh. 

Sheikh Siraj Salum na Sheikh Mahmoud Salim walijiunga na madrasa hiyo kumpa nguvu Sheikh Abdallah mwaka 1977 wakifundisha tafsiri ya Qur’an, Hadith Sirat na lugha ya Kiarabu. 

Kwa nguvu hii mpya darasa lilipata watoto wengi zaidi ambapo ilibidi wasome kwa kupokezana –asubuhi, mchana na wale wa jioni. Mwaka 1984 Mwalimu Abdallah alifariki na hivyo nafasi yake kuchukuliwa na Mwalimu Juma Salim Teva. 

Ongezeko kubwa la wanafunzi lilifanya nafasi kuwa ndogo na hivyo ikawa watoto baadhi wakawa wanasomea nyumbani kwa Sheikh na wengine msikitini. 

Mwaka 1987 Waislamu waliamua kujenga msikiti mpya mkubwa kwa kujitegemea ujenzi ambao ulikamilika mwaka 1992 kwa gharama isiyopungua milioni 55. 

Hivi sasa, Waislamu hao wa Ngaranaro – Unga Limied wapo katika ujenziwa jengo la madarasa lenye ghorofa nne (4) kwa gharama inayokisiwa kufikia shilingi milioni tisini (90 m. shs.) 

Hatua ya awali ya kuweka msingi na kusimamisha nguzo ishakamilika kwa gharama ya shilingi 8,440,000. 

Hata hivyo, ujenzi umesimama toka Februari 1998 kutokana na ukosefu wa fedha na vifaa ambavyo ni vyuma; simenti na mchanga. 

Jengo hilo litakapokamilika litakuwa na vyumba vya madarasa vya kutosheleza shule ya awali ya watoto; madrasa (traditional) na shule ya sekondari. 

Kamati inayosimamia madarasa; msikiti na Ujenzi wa jengo jipya inawaomba Waislamu watoe michango yao kusaidia ujenzi. Michango ya vifaa iwasilishwe msikitini na ile ya fedha itumwe msikiti wa Ijumaa Ngaranaro, 

A/C No. 6590900131 
N.B.C. (1997) Ltd. 
Uhuru Branch Arusha. 

Miongoni mwa mafanikio makubwa ambayo madrasa hii imepata ni pamoja na kutoa wanafunzi wengi sasa hivi ni masheikh, maimamu na waalimu wa madrasa. Miongoni mwao wakiwemo masheikh maarfu kama SheikhYahya Khamis.; Sheikh Adil, Ustaadh Hamidu Issa na Ustadh Abbas Othman. 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI 

Maoni yetu: Prof. Juma Kapuya, vipi Muislamu usijue agenda za Waislamu? 

Hatimaye Mzee Katambo, Chata waachiwa
Na Mwandishi wetu

Polisi Newala wajenga Msikiti 

Sheikh Bafadhil aitaka Bakwata iwe mtetezi wa Waislamu
Na mwandishi wetu

Makala: Uinjilisti wa Mbuni haufai
Na Rajabu Mbambwa, Kigoma

Mussa Katambo: Mzee aliyewekwa rumande kwa kuandaa mihadhara

Ukweli usiachwe 

Makala: Elimu ya ngono yapenyezwa tena Zanzibar 
Na Saidi Mzee 

Arusha wasema: Hongera Mhe. KK kwa kuwa mfano mwema 
Na Hussein M.,  Arusha 

Wanawake Songea kuandaa maonesho 
Na. Jumah Mbwana, Songea 

Kesi ya mgogoro wa Ardhi
Na. Mustafa Adam 

AN-NUUR marufuku gerezani? 
Na Mwandishi Wetu 

Waislamu Karagwe wadai kusalishwa na imamu asiyejua kutawadha 
Na. Abu Abdallah 

Ofisi mpya za Rabita 
Na Mwandishi Wetu

Barua za wasomaji

Habari za Madrasa

Masomo
 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita