AN-NUUR
Na.157 Rabi' Awal 1419, Julai 10 - 16, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Mussa Katambo: Mzee aliyewekwa rumande kwa kuandaa mihadhara 

MZEE Mussa Katambo alizaliwa mwaka 1916 katika kijiji cha Tindiga wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro. Alisoma madrasa moja kwa Sheikh Abdulrahmani Swedi, mkoani Morogoro, 1922. 

Alipigana vita vya pili vya dunia nchini Madagascar 1930, pia alishiriki katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika. 

Hakufanya kazi serikalini wala katika chama. 

Alifanya kazi ya udereva Idara ya Forodha hadi 1980. 

Ndiye muasisi wa Msikiti wa Kibo (Masjid Baytul Muqaddas). 

Aliuza raslimali zake nyingi na kununua kiwanja na kisha kujenga Msikiti huo, pia ni muasisi wa madrasa huko Kisaki- Morogoro, Gomero – Chalinze na sehemu nyingi nyinginezo. 

Alikamatwa mara ya kwanza na polisi akiwa jukwaani akifungua mhadhara wa Khidmat ndani ya eneo la Msikiti wa Kibo hapo Februari 9, 1998 na kupelekwa kituo cha polisi cha Oysterbay kwa kuhojiwa na kisha aliruhusiwa kurudi nyumbani. 

Siku ya pili yake, Februari 10, 1998 alikamatwa nyumbani kwake Ubungo Kibo na kupelekwa moja kwa hadi Kituo Kikuu cha Polisi (Central Police Station) na kuwekwa ndani. 

Kesho yake, yaani Februari 11, 1998 pamoja na waumini wengine walifikishwa kwa mara ya kwanza mahakama ya Kisutu na kusomewa shitaka la kufanya mhadhara bila kibali cha polisi, kukashifu Ukristo kwa kusema "Yesu siyo Mtoto wa Mungu na Biblia siyo kitabu cha kweli". 

Baada ya hapo walipelekwa moja kwa moja katika gereza la Keko. 

Mara walipoingizwa gerezani hapo, walivuliwa nguo zote na kubaki uchi bila kutenganishwa na watoto wadogo na kuanza kupekuliwa sehemu zote za mwili kutafuta kama wameficha mabomu na silaha nyingine. 

Aliingizwa gerezani akiwa na afya njema, lakini ametoka na maradhi ya ngozi. Ametokwa na vidonda kwa kujikunakuna sana kutokana na mwasho wa mwili anaoupata. 

Kutokana na kuathiriwa kisaikolojia, amevurugikwa na akili. Pia ulimi wake umekuwa mzito kutamka mpaka umsikilize kwa makini. 

Aliwahi kupigwa kofi (kibao) na afisa mmoja wa Magereza wakati akipangwa kuelekea mahakamani. 

Anasema katika maisha yake yote tangu ujana wake hakuwahi kuwekwa ndani kabla ya tukio hili. 

Alidai aliambiwa aachiwe kwa masharti kwamba akitoka abomoe Msikiti na aachane na mihadhara, lakini alikataa na kusema ni heri auliwe au awekwe ndani maisha kuliko kukubli masharti hayo. 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI 

Maoni yetu: Prof. Juma Kapuya, vipi Muislamu usijue agenda za Waislamu? 

Hatimaye Mzee Katambo, Chata waachiwa
Na Mwandishi wetu

Polisi Newala wajenga Msikiti 

Sheikh Bafadhil aitaka Bakwata iwe mtetezi wa Waislamu
Na mwandishi wetu

Makala: Uinjilisti wa Mbuni haufai
Na Rajabu Mbambwa, Kigoma

Mussa Katambo: Mzee aliyewekwa rumande kwa kuandaa mihadhara

Ukweli usiachwe 

Makala: Elimu ya ngono yapenyezwa tena Zanzibar 
Na Saidi Mzee 

Arusha wasema: Hongera Mhe. KK kwa kuwa mfano mwema 
Na Hussein M.,  Arusha 

Wanawake Songea kuandaa maonesho 
Na. Jumah Mbwana, Songea 

Kesi ya mgogoro wa Ardhi
Na. Mustafa Adam 

AN-NUUR marufuku gerezani? 
Na Mwandishi Wetu 

Waislamu Karagwe wadai kusalishwa na imamu asiyejua kutawadha 
Na. Abu Abdallah 

Ofisi mpya za Rabita 
Na Mwandishi Wetu

Barua za wasomaji

Habari za Madrasa

Masomo

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita