|
|
|
Na. Mustafa Adam Kesi inayohusu mgogoro wa ardhi kati ya Waislamu na Wakatoliki ilianza tarehe J, baadaya kuahirishwa Januari kutokana na upande wa Wakatoliki kudai kuwa haukuwa na mashahidi. Januari 7,1998 kesi ilianza huku mashahidi wa R.C. na Hakimu kuamua kusikiliza mashahidi wa upande wa Waislamu. Waliotoa ushahidi kwa upande wa Waislamu walikuwa Mzee Sefu Jaharwa, Mbura Bakari Mleli,Isa Mdoe na Alli Omari Msangi. Kesi iliahirishwa baada ya kuwa mashahidi wa upande wa R.C.kuchelewa ikawa Julai 2,1998 ambapo mshitakiwa Stephano Richard (R.C.) alidai mbele ya Mahakama kuwa eneo linalogombewa ni la R.C. Katika mahojiano yaliyofuatia Bw. Stephano alikiri kwamba eneo linalogombewa lilikuwa la Waislamu ila akadai kwamba lilishataifishwa shule zilipotaifishwa. Hata hivyo upande wa Waislamu uliwasilisha Waraka Na. EDF P1/29/104 wa Wizara ya Elimu wa mwaka 1973 unaobainisha kwamba pamoja na kutaifishwa mashule. Majengo na ardhi hubaki kuwa mali ya wamiliki wa awali. Baada ya mashahidi wote wa upande wa Wakatoliki na Waislamu kutoa maelezo yao na kuhojiwa kesi iliahirishwa hadi Julai 16. Katika tarehe hiyo mahakama itahamia kwenye eneo la tukio Duma. |
Maoni yetu: Prof. Juma Kapuya, vipi Muislamu usijue agenda za Waislamu? Hatimaye Mzee Katambo, Chata waachiwa
Sheikh Bafadhil aitaka Bakwata iwe
mtetezi wa Waislamu
Makala: Uinjilisti wa Mbuni haufai
Mussa Katambo: Mzee aliyewekwa rumande kwa kuandaa mihadhara Makala: Elimu ya ngono yapenyezwa
tena Zanzibar
Arusha wasema: Hongera Mhe. KK kwa
kuwa mfano mwema
Wanawake Songea kuandaa maonesho
Kesi ya mgogoro wa Ardhi
AN-NUUR marufuku
gerezani?
Waislamu Karagwe wadai kusalishwa
na imamu asiyejua kutawadha
Ofisi mpya za Rabita
|