|
|
| Historia:
Form IV
Upinzani dhidi ya Serikali
ya Kiislamu wakati wa Khalifa wa Pili Umar Bin Khatab
Umar aliukagua mji wa Jerusalem. Muda wa swala ulipofika Bishop aliwaruhusu waswali kanisani, lakini Umar aliogopa kuswali humo kusije kuwa hoja ya kuchukua kanisa hilo, hivyo aliswalia nje kwenye ngazi. Hata hapo aliacha maandishi yanayokataza kuchukua sehemu hiyo. Umar akiwa Jerusalem aliweka jiwe la msingi la msikiti unaojulikana kwa jina la msikiti wa Umar wa Jerusalem. Inasadikiwa kuwa msikiti huu umejengwa kwenye uwanja ambao Mtume Yakub alipewa Wahy na lilipojengwa hekalu la Solomon.75 Pamoja na kutekwa Jerusalem Warumi walijaribu kuirejesha Syria katika Himaya yao. Watu wa Jazirah kwa sasa ni sehemu ya magharibi ya iraq walikula njama ya kuwaondoa Waislamu Syria. hericlus alipeleka jeshi lake na wakavamia Hims. Hata hivyo walishindwa na Jazirah ikatekwa chini ya ukamanda wa Ayad bin Ghanam. Kutekwa kwa Misri Misri ilikuwa jimbo la Dola ya Warumi. Warumi waliofukuzwa Palestina Syria walikimbilia Misri, hali hii ilihatarisha usalama wa Dola ya Kiislamu hasa kwa vile Misri iko karibu na miji hiyo. Isitoshe Misri iko karibu na Makka jambo ambalo pia lilihatarisha usalama wa Waislamu. Si hivyo tu bali Alexandria kilikuwa kituo kikubwa cha jeshi la maji la Warumi. Hali kadhalika Misri ilikuwa lango kubwa kati ya Arabuni na Afrika ya kaskazini. Isitoshe Warumi walikuwa wanajitahidi kufanya njama ili wakomboe sehemu zilizotekwa. Sababu hizi zilipelekea kuwavamia Misri mnamo mwaka 18 A.H. sawa na 639 A.D. Waislamu waliiteka ngome ya Warumi ya Fusta. Warumi walipostuka na kupeleka jeshi kubwa kamanda wa jeshi la Kiislamu Amr bin al-As alipata askari wengine kutoka kwa Khalifa na walielekea alexandria. Mji huu ulizingirwa kwa miezi sita hatimae ukatekwa na Waislamu mwaka 642 A.C. na baadhi ya wanahistoria wanasema ulitekwa 640 A.D. sawa na 20 A.H. Baada ya ushindi huu Misri ikawa chini ya Himaya ya Kiislamu. Hivi ndivyo vitimvi vya Warumi na Wapeshia wakati wa Ukhalifa wa Umar. Umar alifariki 23 A.H. sawa na (643 A.C.) akiwa na umri wa miaka 61 (sitini na moja). Palikuwa na mtumwa wa Kiajemi aliyemlalamikia tajiri yake kwa Khalifa kuwa anamfanyisha kazi ngumu. Madai haya yalikuwa uongo na Khalifa Umar aliyadharau. Mtumwa huy anaeitwa Lu-Lu-Firoze alijificha katika pembe moja ya msikiti. Na Khalifa alipokuwa anakwenda kuswali alfajir alivamiwa na kupigwa majambia mara sita na mtumwa huyu. Ingawa watu walimkamata lakini alijiua na jambia lile lile. Asubuhi yake al-Faruq Umar Kamanda wa waumini alifariki. Upinzani dhidi ya Serikali ya Kiislam wakati wa Khalifa wa tatu, Uthman bin Affan Wakati wa ukhalifa wa Uthman upinzani ulitokea kutoka kwa Warumi, Wapeshia na kutoka Waislamu wenyewe. Kama ilivyokwisha elezwa uthman alianza ukhalifa tangu mwaka 24 A.H. na akauliwa mnamo mwaka 36 A.H. sawa na (644-656 A.D.). Hali kadhalika tumeshaeleza alivyo chaguliwa na kuwa Khalifa. Upinzani toka kwa Waajemi na Warumi Maadui wa nje Warumi na Wapeshia hawakuwa na sababu mpya za kuendeleza upinzani ila kwa sasa waliendeleza upinzani ili kukomboa sehemu zao zilizotekwa. Tangu wakati wa mtume (s.a.w.) hadi wakati wa umar, Warumi waliipoteza Syria, na Alexandria na Misri. Warumi waliiangalia Syria na Alexandria kwa jicho la wivu na wasingevumilia kuziachia hivi hivi. Hivyo mnamo mwaka 25 A.H. sawa 645 A.C. kulikuwa na maasi makubwa katika mji wa Alexandria yalichochochewa na Warumi, na katika mwaka 26 A.H. Warumi wakavamia alezandria na kuurudisha mikononi mwao. Kahlifa Uthman alipopata taarifa hii alimuamuru kamanda Amr bin al-As kuzima uasi na kuyafukuza majeshi ya Warumi. Kamanda amr aliwashambulia Warumi na kuwafukuza nje ya Alexandria na kwa mara nyingine Alexandria ikawa chini ya Dola ya Kiislamu. Hata hivyo Warumi hawakukata tamaa walivamia tena mji wa Alexandria na jeshi la wanamaji lenye meli 500 mnamo mwaka wa 31 A.H. sawa na 651 A.C. Waislamu hao walijiandaa Muawiya gavana wa jimbo la Syria tayari nae alikuwa na jeshi la wanamaji. Hivyo alituma jeshi lake la wanamaji chini ya ukamanda wa Abdullah bin Sarah na wakapambana baharini. Vita hivi vya wanamaji ndivyo vilikuwa vya kwanza katika historia ya Uislamu. Ingawa Waislamu walikuwa wageni kwenye vita vya majini, haikuwawia vigumu kuwadhinda adui ambao walikimbilia kisiwa cha Cicily. Kwa kuimarisha usalama wa jimbo la Misri na Dola ya Kiislamu kwa ujumla, ilikuwa lazima kwa Waislamu kuiteka ngome kubwa ya Warumi iliyokuwa Tripoli (kwa sasa Libya). Kwa sababu hii Abdullah bin Sarah alipoteuliwa kuwa gavana wa jimbo la Misri, aliomba ruhusa kwa Khalifa Uthman aitwae ngome ya Warumi iliyoko Tripoli. Baada ya mapigano na wakazi wa Tripoli walikubali suluhu kulipa Jizya ya Dirham milioni mbili na nusu kwa mwaka. Mapigano baina ya jeshi la Warumi na Waislamu yalifanyika mahali paitwapo Yaquba. Lakini kamanda wa upande wa adui akauawa na majeshi ya Warumi yakashindwa. kwa ushindi huu Waislamu waliteka sehemu za tunisia, Morocco na sehemu ya Algeria. Uasi wa Azerbaijan na Armenia Mnamo mwaka wa 26 A.H. kulitokea maasi katika jimbola Azerbaijan dhidi ya serikali ya Kiislamu, jimbo hili lilikuwa chini ya Himaya ya Kiislamu tangu wakati wa Umar. Khalifa Uthman alimuamuru Walid bin Uqba gavana wa kufa kuzima uasi wa Azerbaijan. Katika mwaka huo huo watu wa Armenia waliokuwa chini ya Dola ya Kiislamu
tangu wakati wa Umar waliasi. Amir Muawiya Gavana wa Syria alipeleka jeshi
Armenia kukutana na Warumi. Mfalme wa Warumi Constantine II alituma jeshi
la watu 80,000. Kuona hali hii Muawiya aliomba msaada wa Askari kutoka
kwa Khalifa uthman. Jeshi likatumwa chini ya ukamanda wa Habib bin Muslimah,
katika mapigano haya Warumi walishindwa na Armenia ikatekwa. Baada ya ushindi
huu Waislamu waliteka karibu Asia Minor yote pamoja na Aran na Garjastan.
|
YALIYOMO
Tahariri Onyesheni ushujaa wa Badri Daniel kuwatimua waumini Msikitini Waislamu Moshi: Wadai kulishwa nguruwe, vibudu Dondoo za Kisakolojia
Maulana Sayyid Jamal-Din Afghan 1214 - 1254 (1838-1897) - 2 MASHAMBULIZI YA MAREKANI NCHINI IRAQ Njia bora zitakazotusaidia kuwalea
watoto
Ijue Madrasatul-Qaadiriya Sokoni
I Arusha.
Tutafute kwanza ufalme wa Allah (s.w.)
Chuo cha Kilimo Ukiriguru kupata
Msikiti mpya
Huduma za maji Kondoa haziridhishi
Mnyororo wa imani
Je, Yesu alibatizwa?
Kufuatia Waislamu kuritadishwa Merela Morogoro: Masheikh wa mjini watupiwa lawama Abiria walaani kumwagiwa pombe Kondoa Sheikh Bafadhil ateuliwa
kudhamini waandishi wa habari Morogoro
Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|