AN-NUUR 
Na.183 Ramadhan 1419, Januari 8 - 14, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Waislamu Moshi: 

Wadai kulishwa nguruwe, vibudu 
 

  • Sheikh azunguka mjini kuwaandaa Waislamu
  • Kauli ya Sarungi kuamua amani au mapambano
WAISLAMU Mjini Moshi wamedai kwamba wamekuwa wakilishwa nguruwe kwa makusudi kutokana na utaratibu wa Halmashauri ya Wilaya wa kusimamia machinjio ya nyama usiojali uwepo wa Waislamu. 

Wamedai kwamba umekuwepo utaratibu wa mganga mmoja wa nyama kupima nyama ya ng’ombe, mbuzi na nguruwe kwa wakati mmoja na bila kubadili vifaa. Kwa utaratibu huo wamedai kwamba muhuri unaotumika kuwekea alama nyama ya nguruwe ndio huo huo hutumika kwa nyama ya ng’ombe na mbuzi. 

Kutokana na madai hayo, Katibu wa Bakwata Wilaya ya Moshi Mjini Sheikh Mnyone amekuwa akizungukia Misikiti yote mjini Moshi kuwaeleza Waislamu juu ya hali hiyo na kutafakari pamoja nini cha kufanya. 

ANNUUR ilipowasiliana na ofisi husika; madai hayo yalikanushwa na kutolewa maelezo kwamba kuna waganga wawili na mihuri tofauti kwa nyama ya nguruwe. Hata hivyo madai hayo yalipingwa na Bw. Mnyone akisisitiza kwamba muhuri ni mmoja labda wabadili sasa baada ya malalamiko haya. 

Kwa mujibu wa maelezo ya Sheikh Mnyone, madai mengine ya Waislamu ni kuwa machinjio ya nguruwe yapo karibu na makaburi ya Waislamu ambapo uchafu wa wanyama hao hutupwa makaburini hapo. 

Aidha, nguruwe hao wanapoletwa kuuliwa huachwa wavinjari katika makaburi ya Waislamu. 

Jambo jingine lililotajwa kama kero ni uchomaji wa mishikaki ya nguruwe karibu na Msikiti wa Suni na hoteli nyingine za kawaida. Vile vile imeelezwa kwamba kufunguliwa kwa mabucha ya nyama ya nguruwe karibu kabisa na kituo cha mabasi cha Kiboriloni ni kero nyingine. Walalamikaji wanadai ama kituo cha basi kihame eneo hilo au mabucha. 

Kufuatia kero hizo, Katibu wa Bakwata Wilaya amekuwa akiwasilana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkoa ili kutafuta ufumbuzi. 

Uchunguzi wa gazeti hili umegundua kuwa Mkurugenzi huyo alishapelekewa barua tatu toka mwezi Agosti, 1998 kuhusu suala hili. 

Kutokana na Ofisi ya Mkurugenzi kutokuchukua hatua yoyote; Katibu wa Bakwata Desemba 21, 1998 alimwandikia barua Mkuu wa Mkoa Mh. Philemon Sarungi akimwomba aingilie kati suala hili. 

Katika ziara zake Misikitini, Katibu wa Bakwata Sheikh Mnyone amekuwa akikabiliwa na wakati mgumu ambapo Waislamu wamekuwa wakidai ni kwanini halijafanyika jambo la kutoa fundisho kwa Mkurugenzi na wenye machinjio ya nguruwe. 

Hata hivyo, Sheikh Mnyone amekuwa akiwapoza Waislamu na kuwataka wasubiri majibu ya Mkuu wa Mkoa. 

Katika maelezo mengine imedaiwa kwamba upo wasiwasi wa watu kulishwa vibudu kwani Halmashauri imekuwa ikiteua wachinjaji bila kuwashirikisha viongozi wa dini. 

Wasiwasi uliopo ni juu ya umakini na uadilifu wa watu wanaoteuliwa na Halmashauri kuchinja kama hawawezi kutumika "kuhalalisha" kilichokufa bila kuchinjwa. Ombi la Bakwata ni kwamba ishirikishwe kuwateua wachinjaji ili kuondoa wasiwasi wa kulishwa vibudu. 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Tahariri 
Onyesheni ushujaa wa Badri 

Daniel kuwatimua waumini Msikitini 

Waislamu Moshi: Wadai kulishwa nguruwe, vibudu 

Dondoo za Kisakolojia 
Na. Abu Halima Sachangwa 

Kona ya WachaMungu  

Jicho la Uzalendo 

Maulana Sayyid Jamal-Din Afghan 1214 - 1254 (1838-1897) - 2 

Vipi umoja wetu uwe hatari ? 

MASHAMBULIZI YA MAREKANI NCHINI IRAQ  

Marekani si rafiki mwema  

Tunahitaji UN ya Waislamu - 2  

Njia bora zitakazotusaidia kuwalea watoto 
Na Ust. Hashim Rusaganya, Mombasa 

Ijue Madrasatul-Qaadiriya Sokoni I Arusha. 
Na Habiba Swedi, Arusha 

Tutafute kwanza ufalme wa Allah (s.w.) 
Na Mwapwani Mohammed 

Sheikh Kisiwa atunuku zawadi 

Chuo cha Kilimo Ukiriguru kupata Msikiti mpya  
Na Mwandishi Wetu, Mwanza  

Huduma za maji Kondoa haziridhishi 
Na Abu Zuberi, Kondoa  

Mnyororo wa imani 
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa 

Je, Yesu alibatizwa? 
Na Muhibu Said  

Kufuatia Waislamu kuritadishwa Merela Morogoro: Masheikh wa mjini watupiwa lawama  

Abiria walaani kumwagiwa pombe Kondoa 

Sheikh Bafadhil ateuliwa kudhamini waandishi wa habari Morogoro 
Na Mussa Ally, Morogoro 

Sayansi na Teknolojia 
[Tatizo la mwaka 2000] 

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Chakula na lishe 
[Mlo wa siku ya Idd] 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita