|
|
| Mlo
wa siku ya Idd
Na Mujahid Mwinyimvua IDD - el - Fitr ni sikukuu inayoanza baada ya kumalizika kwa mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Katika makala zetu maalum za chakula na lishe za mwezi huu wa Ramadhani, tulijifunza mlo wa futari na mlo wa daku. Ni vyema pia wiki hii tukajifunza mlo wa siku ya Idd el Fitr. Kwa kawaida mwili wa mwanaadamu huweka akiba ya chakula. Chakula hicho hutumika wakati wa mazingira fulani kama vile pale ambapo mwili wa mwanadamu unapokosa chakula (kipya) yaani mtu akikaa masaa kadhaa bila kula. Funga ya Ramadhani ni mfano wa hali ya mwili kukaa masaa fulani bila ya chakula. Kwa maneno mengine tunaweza kusema kwamba ibada ya funga ya Ramadhani inausaidia mwili kutumia chakula chake cha akiba. Chakula hicho cha akiba kikikaa kwa siku nyingi mwilini bila ya kutumika kinaweza kuleta magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na ulaji (vyakula). Mtu anapomaliza mfungo wa mwezi wa Ramadhani sehemu fulani ya chakula chake cha akiba huwa kimeshatumika, ndiyo maana wengi waliofunga hupungua miili yao. Idi inapoanza mwili wa mtu nao unaanza zoezi jipya la kuweka akiba mpya. Kwa hiyo elimu juu ya mlo gani wa siku ya Idi na siku nyingine zinazofuata ni jambo la msingi. Kwa vile kipindi chote cha Ramadhani mwili umezoea kula usiku tu, ni vyema siku ya Idi iwe na mlo maalum, yaani ule mlo utakaofurahiwa na kila mtu katika familia. Vile vile mlo wa siku ya Id na siku zinazofuata lazima uwe mlo kamili (Balance diet) ili mwili uweze kujijenga upya. Hata hivyo, tusisahau kanuni za lishe kuwa: Kula sana ni chanzo kikubwa cha maradhi mbalimbali kwa binadamu. Inawezekana katika jamii fulani baadhi ya watu wakakosa uwezo wa kupata/kununua chakula kwa ajili ya siku ya Idi. Wasiwasi huo ni mkubwa zaidi tunapoitazama nchi ya Tanzania ambayo karibu nusu yake ina njaa kali. Dini ya Kiislamu imeweka sheria (ibada) kwa kila Muislamu mwenye uwezo japo wa kawaida atoe zaka maalum ya funga ya Ramadhani (Zakatul Fitr) na kuwapa wale wasiokuwa na kitu. Kama ibada hiyo itatekelezwa ipasavyo inawezekana hasa siku ya Idi kila mtu (hasa muumini) atakuwa na chakula kizuri na chakutosha na pia ataweza kukidhi mahitaji yake mengine. Tunamalizia makala hii, tukizingatia umuhimu wa lishe bora kwa kuwakumbusha
na kuwaomba Waislamu wenye uwezo (japo akiba ya shilingi mia tano) watowe
zakatul Fitr.
|
YALIYOMO
Tahariri Onyesheni ushujaa wa Badri Daniel kuwatimua waumini Msikitini Waislamu Moshi: Wadai kulishwa nguruwe, vibudu Dondoo za Kisakolojia
Maulana Sayyid Jamal-Din Afghan 1214 - 1254 (1838-1897) - 2 MASHAMBULIZI YA MAREKANI NCHINI IRAQ Njia bora zitakazotusaidia kuwalea
watoto
Ijue Madrasatul-Qaadiriya Sokoni
I Arusha.
Tutafute kwanza ufalme wa Allah (s.w.)
Chuo cha Kilimo Ukiriguru kupata
Msikiti mpya
Huduma za maji Kondoa haziridhishi
Mnyororo wa imani
Je, Yesu alibatizwa?
Kufuatia Waislamu kuritadishwa Merela Morogoro: Masheikh wa mjini watupiwa lawama Abiria walaani kumwagiwa pombe Kondoa Sheikh Bafadhil ateuliwa
kudhamini waandishi wa habari Morogoro
Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|