AN-NUUR 
Na.183 Ramadhan 1419, Januari 8 - 14, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Tunahitaji UN ya Waislamu - 2  

Na Tahir Rashid 

New York: 

Mji maarufu kuliko yote leo duniani, ni mji huu wa New York.Hapo ndipo ambapo Baraza Kuu la Ulimwengu liliposimikwa, nalo ni Baraza la Umoja wa Mataifa. Baraza hili liko katika nyumba ya Umoja wa Mataifa badala ya kuwa katika nyumba isiyo na kushirikisha (22:26). Na haya sio kwa kubahatisha. La. Bali ni mpango maalumu ili watu wageuzwe bila wao kujua. Na imekuwa hivyo. Siri hii New York maana yake ni "Kiini Kipya". Sasa hicho kiini cha kale ni kipi? (22:29) 

Hivi kusema New York kwa maana ya kiini kipya, Waingereza wenyewe wangaliita New Center. Sasa la kujiuliza ni kwamba ni ipi iliyokuwa Old Center? 

Zingatia uone kwamba katika huo mji uitwao New Center ipo nyumba inayoeleweka na walimwengu wote kwa maongozi na baraka (ruzuku). Kwa hiyo, tukisema ipi hiyo Old Center la kuangalia hapa ni kutafuta kuijua nyumba ya kwanza iliyowekwa kwa ajili ya ulimwengu wote (Umoja wa Mataifa wa kweli) yenye maongozi na baraka (3:96). Na jambo hili la uongozi limefichwa. (2:159, 2:146). Uongozi wa walimwengu wote ndio Uongozi (2:120) 

Nyumba hii ya Umoja wa Mataifa bandia iliyoko kiini kipya ndiyo ambayo Mola wetu anaiita "nyumba ya maangamizo". (14:28). Hutuamrisha kuua watoto (6:1379) (Uzazi wa mpango) kwa hiyo utaratibu wa maisha unavurugwa. Lengo la maisha ya watu limekuwa ni kuboresha mazingira yao binafsi bila kujali litakalo tokea. 

Kwa maana hii ituyakinie kwamba hivi leo duniani upande (kibla) watu wanapoelekea sio kiini cha kale (Makkah). Bali ni kiini kipya (New York). Jambo ambalo Mola wetu ametuasa kuwa tusifuate upande (kibla) wa wale waliopewa Kitabu (2:145) kwani tukifanya hivyo, tutakuwa "madhalimu". Kwa kuelekea leo kibla cha New York hakuna maana nyingine bali sisi tulioko Makanisani na Misikitini tumekuwa madhalimu bila kujua. 

Wito wa Allah (s.w.): 

Na Mwenyezi Mungu anatuita katika nyumba ya amani (The Old Center) (10:25) (kwani) amani itakuwa juu ya wale wanaofuata uongozi (Wake) (20:47). Hapo ndipo ilitakiwa liwepo baraza la (Usalama 2:124). 

Jambo ambalo wale waliopewa Kitabu wanalijua kama wanavyo wajua watoto wao (2:146). Lakini kwa dhulma yao (4:160) (huzua kwao kibla kingine 2:145) watu walioko Makanisani na Misikitini, tunafuata kibla hiki, kwa hiyo nasi sote tumekuwa madhalimu. (Ole wetu) siku ambayo itatufikia adhabu aseme wale waliodhulumu. "Mola wetu tuakhirishe muda kidogo, tutaitikia wito wako na tutawafuata Mitume ..." (14:44). Kwani huku kumfuata Mtume ni nini? 

Tujiulize kwanza, hivi leo anayefuatwa ni nani? Mtume leo hayupo, lakini kile alichokuja nacho kipo. Na ni agizo kwetu kuwa tuwaite watu kwa Mola wetu na mtu yeyote asikuzuie kufuata aya za Mwenyezi Mungu (28:87). Na ni nani dhalimu kuliko yule anayekumbushwa aya za Mola wake akawa anazipuuza, na akayasahau yaliyotangulizwa na mikono yake. (18:57) Watu badala ya kukampeni jina kwa ajili ya Allah (s.w.) wao hukampeni kwa ajili ya majina yasiyokuwa jina Hili. Basi wasituzuie (kukampeni kwa ajili ya Rais wetu Allah) wale wasioamini na wafuatao matamanio yao. (20:16). Kwa kufuata matamanio yao (kibla chao 2:145) tumekuwa madhalimu pasipo kujua (30:26). 

Kumfuata Mtume! 

Mwenyezi Mungu aliwatuma Mitume wawili na akawazidishia nguvu kwa Mtume wa tatu; lakini watu waliwakadhibisha (36:14) kwa kuendelea kufuata mila za wakuu wao (7:88-89). Basi akaja mtu akisema "enyi watu wangu wafuateni mitume hawa" (36:20). Kwa sababu kwa kuwafuata Mitume ndio kumuabudu Muumba (36:22). Usipowafuata Mitume utashika Miungu mingine badala Yake (26:23) na huo ndio kuwa katika upotofu uliodhahiri (36:24). Udhalimu maana yake (31:11). Tusijesema "Wallahi", kwa yakini tulikuwa katika upotofu ulio dhahiri, tulipokuwa tukikufanyeni sawa na Allah. Na si wengine hawa wanaofanywa sawa na Allah ila ni (watu) waovu (26:97-99). Nao ni wakuu wa miji (6:123). 

Kwa kuwafuata wakuu wetu wa miji, ndio upotofu uliodhihiri. Kwani wao ofisi zao huelekea Ikulu iliyoko mji mkuu. Na Ikulu hiyo iliyopo mji mkuu imeelekea Ikulu ya dunia iliyoko Kiini Kipya. Hivyo, kwa ulaini maongozi ya Allah yametiwa kapuni. Ni kwa kuelekea Ikulu ya dunia iliyoko Makkah ndio Kumfuata Mtume (2:44) ili tuongoke (2:150). 

Said Rajab. Nyanyua mikono tuombe, kwani si mwingine bali ni wewe uloleta hoja hii adhimu. "Mola wetu tumesikia na tutatii tunakuomba msamaha. Na marejeo ni kwako. (2:285). Mola wetu usizipotoe nyoyo zetu baada ya kutuongoza na utupe rehema itakayo kwako. (Wallah jambo hili la mji mkuu wa dunia (Makkah) limefichwa) hakika Wewe ndiye Mpaji Mkuu (3:8). Mola wetu usiendelee kututesa kwa kusahau kwetu (tukakosea na kufuata maongozi ya New York). Hivyo, usitubebeshe mgizo kama ulivyowabebesha wale waliokuwa kabla yetu. Usitutwike tusiyoyaweza, na utusamehe, na utughufirie, na uturehemu. Wewe ndiye Mlinzi wetu. Basi tusaidie juu ya makafiri. (2:286). Hali yetu ni mbaya. Tuko Misikitini na Makanisani na tunafanywa kugombana, kumbe kikulacho kiko nguoni mwako. 

AMIN 

Inaendelea toleo lijalo  
 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Tahariri 
Onyesheni ushujaa wa Badri 

Daniel kuwatimua waumini Msikitini 

Waislamu Moshi: Wadai kulishwa nguruwe, vibudu 

Dondoo za Kisakolojia 
Na. Abu Halima Sachangwa 

Kona ya WachaMungu  

Jicho la Uzalendo 

Maulana Sayyid Jamal-Din Afghan 1214 - 1254 (1838-1897) - 2 

Vipi umoja wetu uwe hatari ? 

MASHAMBULIZI YA MAREKANI NCHINI IRAQ  

Marekani si rafiki mwema  

Tunahitaji UN ya Waislamu - 2  

Njia bora zitakazotusaidia kuwalea watoto 
Na Ust. Hashim Rusaganya, Mombasa 

Ijue Madrasatul-Qaadiriya Sokoni I Arusha. 
Na Habiba Swedi, Arusha 

Tutafute kwanza ufalme wa Allah (s.w.) 
Na Mwapwani Mohammed 

Sheikh Kisiwa atunuku zawadi 

Chuo cha Kilimo Ukiriguru kupata Msikiti mpya  
Na Mwandishi Wetu, Mwanza  

Huduma za maji Kondoa haziridhishi 
Na Abu Zuberi, Kondoa  

Mnyororo wa imani 
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa 

Je, Yesu alibatizwa? 
Na Muhibu Said  

Kufuatia Waislamu kuritadishwa Merela Morogoro: Masheikh wa mjini watupiwa lawama  

Abiria walaani kumwagiwa pombe Kondoa 

Sheikh Bafadhil ateuliwa kudhamini waandishi wa habari Morogoro 
Na Mussa Ally, Morogoro 

Sayansi na Teknolojia 
[Tatizo la mwaka 2000] 

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Chakula na lishe 
[Mlo wa siku ya Idd] 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita