AN-NUUR 
Na.183 Ramadhan 1419, Januari 8 - 14, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Kugeuzwa nyumba za Wakfu Baa, sasa... 

Daniel kuwatimua waumini Msikitini 
 

  • Adai hawamlipi kodi
  • Kamishna wa Ardhi kuombwa ampe hati mpya
BW. DANIEL Zakaria aliyepewa usimamizi wa Mirathi ya nyumba za Wakfu na mahakama; sasa anaiomba mahakama iwatimue waumini wa Masjid Mwinyi akidai kwamba hawamlipi kodi yake. 

Masjid Mwinyi umejengwa katika kiwanja ilipokuwa moja ya nyumba za marehemu Hajat Aziza Omar - Kiwanja Na. 23 kitalu K. No. 66 mtaa wa Moshi. 

Kutokana na usimamizi aliopewa na Hakimu Natalia Kimaro juu ya nyumba hizo za Wakfu Bw. Daniel anadai kwamba hata Masjid Mwinyi ni mali yake kwa hiyo kama waumini wanataka kuendelea kuswali hapo walipe kodi. 

Akipigania kupata kodi yake kupitia mahakama ya Kisutu hivi karibuni; Bw. Daniel aliiambia mahakama kupitia maandishi: "Naiomba Mahakama itoe Eviction Order ya kusimamisha ibada katika kiwanja Na. 23 Kitalu K. No. 66 Moshi Street Ilala." 

Akielezea sababu ya kuomba mahakama iwatimue waumini Msikitini hapo alisema kwamba waumini hao "gharama wanazozitumia hawazilipii (ikiwa ni) jengo lenyewe, kiwanja, maji na umeme". Akaongeza "maswala hayo yanafanya nisimamishe shughuli za Ibada". 

Kabla ya hatua hii ya kuitaka mahakama iwatimue waumini; Julai 2, 1998 Bw. Daniel aliiomba Ofisi ya Ardhi Kanda ya Ilala imkabidhi nakala ya barua ya toleo (offer) ya kiwanja hicho cha Msikiti ambayo ilitolewa kwa jina la Aziza Omar. 

Suala hilo lilikuwa gumu kwa Afisa Ardhi Bw. J.M. Mahela kwa hiyo akamshauri Bw. Daniel Zakaria amuombe Kamishna wa Ardhi atengue barua ya toleo kwa jina la marehemu Aziza Omar. 

Kwa mujibu wa maelezo ya Bw. Ardhi huyo kama yalivyo kwenye barua No. ILA/3632/14 ya Julai 28, 1998, barua mpya ya toleo (offer) yaweza kutolewa kwa jina la Bw. Daniel baada ya Kamishna kutengua ile ya awali. 

Ukiacha Msikiti, Bw. Daniel alishachukua nyumba nyingine mbili za Wakfu ambazo zipo Mtaa wa Somali No. 58 Gerezani na Mchikichi No. 59 Kariakoo. 

Nyumba hizo ziliwekwa Wakfu na Hajat Aziza Omar kwa hati ya kiapo MCA/284 2/84 Mahakama ya Mwanzo ya Kariakoo Oktoba 11, 1990. 

Kwa kauli ya maandishi Hajat Aziza alisema "Natoa wosia nikifa nyumba hizo ziwe WAKFU kwa ajili ya MASJID MWINYI uliopo No. 66 MOSHI STR ILALA D’SALAAM". 

Pamekuwa na wasiwasi miongoni mwa waumini juu ya ushirikiano uliopo baina ya Bw. Daniel Zakaria na baadhi ya wasimamizi wa nyumba za Wakfu za Hajat Aziza. 

Wasiwasi huo umekuja kwa kuona kwamba pamekuwa na uzito wa kuchukua hatua stahiki hadi Bw. Daniel anathubutu kuweka Baa kwenye nyumba ya Wakfu. 

Waumini mbalimbali ambao waliongea na gazeti hili walisema kwamba hawaelewi ni kwanini Masheikh hao wasimamizi wa Wakfu hawajafungua kesi kupinga hukumu ya Hakimu Natalia Kimaro kumpa Bw. Daniel usimamizi wa nyumba za Wakfu. 

Wala hawaelewi ni kwanini kama wameshindwa kukabiliana na Bw. Daniel kwa sababu yoyote iwayo hawajawaita Waislamu wa Dar es Salaam wakawakabidhi jukumu hilo. 

Hata hivyo wamesema kwamba iwe vyovyote iwavyo maadhali wana uhakika kuwa hizo ni nyumba za Wakfu hatakaa Daniel wala atakayeuziwa nyumba hizo na Danie 

Magereza yashukuru misaada ya Jumuiya ya Kiislamu 

JESHI la Magereza mkoani Morogoro limeishukuru Jumuiya ya Islamic Foundation ya mjini hapa kutokana na misaada mbalimbali iliyoitoa kwa wafungwa wa magereza kadhaa ya mji huu. 

Katika barua zao kwa Mudir wa Islamic Foundation, Sheikh Suleiman Kiriri zilizoandikwa kwa nyakati tofauti, viongozi wa Magereza hayo pamoja na kuipongeza jumuiya hiyo, waliiomba iendelee kuwasaidia wafungwa na kuwaomba Waislamu popote pale walipo kuiga mfano huo. 

Misaada iliyotolewa na jumuiya hiyo ni pamoja na Hijab kwa wafungwa wote Waislamu wa gereza la wanawake Kingorwila, madawa yenye thamani ya shilingi 150,000 kwa wafungwa waliopata tohara katika gereza la Mtego wa Simba na msaada wa futari na daku kwa magereza saba yenye jumla ya wafungwa 206 waliofunga. 

Magereza hayo ni Mtego wa Simba, Mkono wa Mara, wanawake Kingoruwila, mahabusu Morogoro mjini, Mbigiri, Wamikuu na Wami Vijana. 

Misaada mingine iliyotolewa na Islamic Foundation ni ujenzi wa Msikiti na nyumba ya mwalimu katika gereza la Mtego wa Simba. 

Katika barua yake ya Desemba 27, 1998 yenye kumbukumbu nambari 166/Moro/3/84 kwa Islamic Foundation, Mkuu wa Gereza la wanawake ASP Angela ameomba ushirikiano wa gereza lake na jumuiya hiyo ya Kiislamu usiishie tu katika mwezi huu wa Ramadhani bali wakati wowote nafasi itakaporuhusu. 

Naye Mwenyekiti wa Msikiti wa Magereza Mtego wa Simba Bw. Juma Lipalala katika barua yake yenye Kumbukumbu nambari 166/Moro/1/379 kupitia kwa Mkuu wa gereza hilo Bw. Ruvugo aliiomba Islamic Foundation pamoja na Waislamu wengine kuendelea kuwasaidia wafungwa magerezani, hali ambayo si tu itawafariji bali pia itasaidia kubadili tabia zao. 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Tahariri 
Onyesheni ushujaa wa Badri 

Daniel kuwatimua waumini Msikitini 

Waislamu Moshi: Wadai kulishwa nguruwe, vibudu 

Dondoo za Kisakolojia 
Na. Abu Halima Sachangwa 

Kona ya WachaMungu  

Jicho la Uzalendo 

Maulana Sayyid Jamal-Din Afghan 1214 - 1254 (1838-1897) - 2 

Vipi umoja wetu uwe hatari ? 

MASHAMBULIZI YA MAREKANI NCHINI IRAQ  

Marekani si rafiki mwema  

Tunahitaji UN ya Waislamu - 2  

Njia bora zitakazotusaidia kuwalea watoto 
Na Ust. Hashim Rusaganya, Mombasa 

Ijue Madrasatul-Qaadiriya Sokoni I Arusha. 
Na Habiba Swedi, Arusha 

Tutafute kwanza ufalme wa Allah (s.w.) 
Na Mwapwani Mohammed 

Sheikh Kisiwa atunuku zawadi 

Chuo cha Kilimo Ukiriguru kupata Msikiti mpya  
Na Mwandishi Wetu, Mwanza  

Huduma za maji Kondoa haziridhishi 
Na Abu Zuberi, Kondoa  

Mnyororo wa imani 
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa 

Je, Yesu alibatizwa? 
Na Muhibu Said  

Kufuatia Waislamu kuritadishwa Merela Morogoro: Masheikh wa mjini watupiwa lawama  

Abiria walaani kumwagiwa pombe Kondoa 

Sheikh Bafadhil ateuliwa kudhamini waandishi wa habari Morogoro 
Na Mussa Ally, Morogoro 

Sayansi na Teknolojia 
[Tatizo la mwaka 2000] 

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Chakula na lishe 
[Mlo wa siku ya Idd] 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita