AN-NUUR 
Na.188 Shawwal 1419, Februari 12 - 18 , 1999 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Askari wa Tume ya Jiji wapora mkaa
 

ASKARI wa Tume ya Jiji la Dar es Salaam wamelalamikiwa kwa kuchukua mkaa wa mfanyabiashara hiyo katika eneo la Msasani Mikoroshoni Jijini hivi karibuni. 

Akiongea na mwandishi wa habari hizi, Bw. Ally Kasinge ambaye ndiye mmiliki wa biashara hiyo ameeleza kuwa Februari 4 mwaka huu askari hao wa Tume ya Jiji walivamia eneo lake la biashara na kupora magunia 46 ya mkaa kwa madai kuwa hakuwa na leseni ya kufanya biashara katika eneo hilo. 

Bw. Ally amesema kuwa wakati hayo yanafanyika yeye alikuwa amekwenda kunywa chai na kuwaachia vijana wawili kumtizamia biashara yake, vijana hao aliwataja kuwa ni Bw. Salum Athumani na Yahya Mohamed walipelekwa katika mahakama ya Tume ya Jiji na kila mmoja kuandikiwa kuwa amekutwa na gunia mbili za mkaa na hivyo kutozwa faini ya shilingi 10,000 kila mmoja. 

Bw. Ally ameendelea kueleza kuwa baada ya kulipa faini hizo bado hakurudishiwa mkaa wake na alipojaribu kufuatilia kwa Mkuu wa Mkoa alitakiwa kwanza apitie ofisi za Mkuu wa wilaya. 

Amesema aliporudi wilayani kuelezea kile alichotendewa na askari wa Tume ya Jiji aliambiwa kama haridhiki afuatilie ngazi nyingine. 

Bw. Ally amesema kuwa anaona haki yake inapotea na hivyo anaomba vyombo vinavyohusika kumsaidia ili aweze kupata haki yake kwani anachosema ni kwamba wafanya biashara wote wa mkaa katika eneo la Msasani Mkoroshoni hawana leseni lakini yeye peke yake ndiyo aliyekamatwa. 

Suala la askari wa Jiji kuwavamia wafanyabiashara ndogondogo hapa jijini limekuwa likishamiri kwa kasi kubwa katika siku za karibuni. 

Jitihada za kumpata Mwenyekiti wa Tume ya Jiji kuhusiana na suala hili hazikufanikiwa hadi gazeti hili linakwenda mitamboni wiki hii. 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
  

Tahari 
Tusirudishane nyuma 

Mwaka mmoja wa mauaji ya Mwembechai: Waliouawa ni wanne
Na Mwandishi wetu

Waasisi wa TAA waibuka kupigania haki zilizoporwa

Kuhujumiwa Waislamu kielimu: Mzazi adai mwanafunzi Adam Rashid kafelishwa

Maoni yetu: Tuondoleeni wenye mikono ya damu

MARADHI YA KISAIKOLOJIA: MULTIPARAPHILIASIS

Askari wa Tume ya Jiji wapora mkaa

Kuchangia Radio Kheri Broadcasting Station

Yesu Kristo na Yohana Mbatizaji
Na BERNARD B. MWENDA

Wakereketwa CCM wawakosha wauaji wa Mwembechai
Na Idd Kikong’ona, Morogoro

Ufugaji holela wa nguruwe waikumba Dodoma
Na Abu Zubeir, Dodoma

Watembelea na kusaidia wagonjwa Arusha

Mkuu wa wilaya awatimua Masheikh ofisini kwake
Na Mwandishi Wetu, Morogoro

Kutoka magazeti ya zamani

Sayansi na Teknolojia 
[Windows: Mambo Mazuri ya Kuyajua] 

Masomo ya Kiislam 

Barua za Wasomaji 

Mashairi

Chakula na Lishe 
[Kauli hii ya serikali itatumaliza Watanzania kwa njaa] 

Kumbukumbu ya mauaji Mwembechai 
[Maazimio ya Maimamu Dar]
 
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita