AN-NUUR 
Na.188 Shawwal 1419, Februari 12 - 18 , 1999 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Maoni yetu
 
 
Tuondoleeni wenye mikono ya damu
  

KATIKA miaka ya awali ya maisha ya Utume ya Mtume (s.a.w.) Waislamu walipata mateso makubwa sana. Zaidi mateso hayo yaliongozwa na waliokuwa wakuu wa koo za Kiquraysh na wale wa dini za kishirikina. 

Abujahal aliyekuwa mmoja wa makamanda wa kikosi cha kuwatesa Waislamu aliongoza mashambulizi dhidi ya Waislamu dhaifu ambao hawakuwa na silaha. 

Hamza ambaye alikuwa miongoni mwa viongozi walioheshimiwa sana na ambaye alikuwa pia hajasilimu alipofika kwenye tukio hilo hakuweza kuhimili kuona watu wasio na silaha wakiteswa. 

Alimnasa kibao kamanda Abujahal na ‘askari’ wale watesaji kila mmoja akasambaa katika njia tofauti. 

Hizo zilikuwa zama zilizoitwa za ujahili ambapo sifa ya kabila au taifa ilitegemea uwezo wake wa kupigana, kuua na kupora mali toka kabila jingine. Zilikuwa zama za kuzika watoto wa kike wakiwa hai. 

Karne kumi na tano baadae Waislamu wasio na silaha wameuliwa na polisi kwa amri ya Kamanda wao. Kama walivyokuwa dhaifu Waislamu wale wa wakati wa Kamanda Abujahal Waislamu hawa wa Tanzania huru kwa udhaifu wao wanalinganishwa na watoto ambao "bado wananyonya". Lakini hata hivyo wanapigwa risasi na kuuliwa. 

Miaka 1500 iliyopita alipatikana Hamza aliyewatetea na kumtia adabu Kamanda anayeua watu wasio na silaha. Leo Makamanda wanapongezwa na wakuu wa nchi! 

Zile zilikuwa zama za kiza. Leo ni zama za kupigania haki za binadamu, zama za demokrasia, zama za serikali zinazowekwa na watu kwa ajili ya watu! Lakini leo wauaji wanapongezwa wakati zama za kiza walilaaniwa na kutiwa adabu. 

Wahshiy alikuwa mtumwa wa Hind bint Utbah mke wa Abu Sufyani. Katika vita vya Uhud Wahshiy alipewa amri amsake Hamza mpaka amuue. Na kweli akamuua. 

Baadaye Wahshiy alisilimu, hata hivyo ikawa kila Waislamu wakikutana naye humkumkumbuka Hamza na kupata majonzi. Mtume (s.a.w.) akamwamuru ahamie mji mwingine wa mbali. 

Leo sisi tuna akina Wahshiy ambao hawakuamrishwa kitumwa wala hawakuwa vitani; bado tupo nao. Baya zaidi wanazidi kutukejeli kwa kutuhubiria upendo, amani na usalama. 

Ni vyema serikali angalau ikajali hisia zetu ikatuondolea Wahshiyi hawa machoni petu. 

Kila tusikiapo sauti zao na kuwatia machoni kwenye majukwaa ya kisiasa au maofisini mwao wanatuletea majonzi kwa wenzetu waliouliwa Mwembechai. 

Juu 
 

YALIYOMO 
  

Tahari 
Tusirudishane nyuma 

Mwaka mmoja wa mauaji ya Mwembechai: Waliouawa ni wanne
Na Mwandishi wetu

Waasisi wa TAA waibuka kupigania haki zilizoporwa

Kuhujumiwa Waislamu kielimu: Mzazi adai mwanafunzi Adam Rashid kafelishwa

Maoni yetu: Tuondoleeni wenye mikono ya damu

MARADHI YA KISAIKOLOJIA: MULTIPARAPHILIASIS

Askari wa Tume ya Jiji wapora mkaa

Kuchangia Radio Kheri Broadcasting Station

Yesu Kristo na Yohana Mbatizaji
Na BERNARD B. MWENDA

Wakereketwa CCM wawakosha wauaji wa Mwembechai
Na Idd Kikong’ona, Morogoro

Ufugaji holela wa nguruwe waikumba Dodoma
Na Abu Zubeir, Dodoma

Watembelea na kusaidia wagonjwa Arusha

Mkuu wa wilaya awatimua Masheikh ofisini kwake
Na Mwandishi Wetu, Morogoro

Kutoka magazeti ya zamani

Sayansi na Teknolojia 
[Windows: Mambo Mazuri ya Kuyajua] 

Masomo ya Kiislam 

Barua za Wasomaji 

Mashairi

Chakula na Lishe 
[Kauli hii ya serikali itatumaliza Watanzania kwa njaa] 

Kumbukumbu ya mauaji Mwembechai 
[Maazimio ya Maimamu Dar]
 
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita