|
|
| Home |
Ashitakiwa baada kusilimuya kusilimuNa Mwandishi Wetu, TangaMFANYAKAZI wa Shirika la Simu Mkoani Tanga, Bwana Salim Songoro ameshtakiwa baada ya kuamua kuacha Ukristo na kuingia Uislamu. Bwana Salim ambaye kabla akijulikana kwa jina la Samwel Manfred Songoro kutoka dhehebu la Kikatoliki, alifikishwa mahakamani kwa mara ya mwanzo mnamo mei 21,1998. Wanaomshtaki ni aliyekuwa Bi. Fausta Mathayo akishirikiana na wazazi wake. Katika shtaka hilo nambari 299/98 kwenye mahakama ya mwanzo; Bwana Salim anadaiwa kuwatelekeza mkewe na watoto wake na kuwawacha bila huduma yoyote. Akizungumza mbele ya Waislamu wenzake Bana Salim amesema kuhusiana na madai hayo, tayari amewahi kushinda rumande, na kwamba kwasasa yuko nje kwa dhamana. Akiendelea kujieleza amekanusha kuwa ati amewatelekeza watoto wake. Pamoja na kwamba hamuhudumii Bi Fausta ambaye si mke wake tena, lakini amewapangishia chumba kwa ajili ya watoto wake watatu aliozaa naye na kuwapa kila msaada chini ya uwezo wake. Huku mshtakiwa akiwa nje kwa dhamana na wazazi wa Fausta wakiwa wamemkamia
vibaya Bwana Salim, Waislamu nao tayari wameanza kuchangishana fedha za
kuendeshea kesi ambayo kwa mara ya pili ilisikilizwa Juni 4,mwaka huu.
|
Maoni yetu:
Unafiki si suala la wakati fulani
Historia ya harakati za ukombozi wa Kashmir Sheikh wa Wilaya Same ahimiza Waislamu kushiriki tamasha Sheikh awataka wanawake wajistiri Madrasat Al-Hujuun washerehekea
mwaka mpya
|
| An-nuur Home | Links | Islam Tanzania | Matoleo yaliyopita |