AN-NUUR
Na.154 Safar 1419, Juni 19-25, 1998
 
Home 

Links 

Islam Tanzania 

Matoleo ya nyuma 
 
 

Wakatoliki wawili wasilimu 

Na Mwandishi Wetu, Mtwara 

WAKATOLIKI wawili Bw. Thomus Matei na Bi. Reinata George wamesilimu Juni 13, mjini Mtwara na kufunga ndoa katika Msikiti wa Ijumaa Chikongola. Waislamu hao wapya walisilimishwa na Sheikh Khamis Mchewa. 

Bw. Thomus Matei hivi sasa anaitwa Bw. Suleiman wakati Bi. Reinata amechukua jina la Zamda. 

Baada ya kusilimu, Waislamu hao wapya waliomba wafungiwe ndoa, Bibie Zamda alidai mahari ya shilingi 6,000, Waislamu walimchangia Bw. Suleiman zaidi ya shilingi 8000 na ndoa kufungwa hapo hapo na Sheikh Jamaldeen Salim. 

Katika nasaha zake kwa Waislamu, Sheikh Jamaldeen aliwahimiza Waislamu kuitangaza dini ya Allah bila ya kuogopa vitisho vya maadui. 

Alisema kwamba kuutangaza Uislamu na kufanya majadiliano juu ya Mungu Mmoja wa Kweli ni amri ya Allah (sw). 

 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI  

Maoni yetu: 
Kama hodari wa kuhoji Tuhoji pia Tume ya Majeshi ya Vita 

Waraka wa Abu Aziz  

Unafiki si suala la wakati fulani  
  
Wakatoliki wawili wasilimu 

Ashitakiwa baada kusilimu 

Historia ya harakati za ukombozi wa Kashmir 

Sheikh wa Wilaya Same ahimiza Waislamu kushiriki tamasha 

Sheikh awataka wanawake wajistiri 

Madrasat Al-Hujuun washerehekea mwaka mpya 
 
Kutoa talaka ovyo ovyo ni kuchupa mipaka ya Allah - Ust. Khamis Salim 

Uislamu ni mfumo wa maisha - Mbukuzi 

Pole ya Mwinjilisti Kusupa ni kejeli 
 

 
 Maoni yoyote kuhusu ukarasa huu yapelekwe kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
An-nuur Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita