AN-NUUR 
Na.172 Rajab 1419, Oktoba 23 - 29, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 
Shairi 

Simlazimishe Yesu ukombozi wa ulimwengu (jibu) 
 

Wapagani itakidi, kwa mungu wao ibadi, 
Ni kuwatoa waladi, chini ya miti na mikadi, 
Zitolewe zamaradi, na kufukiza kwa udi, 
Toleo za kiibadi, Ezekieli shahidi. 

Kumi na sita idadi, ndiyo sura anonadi, 
Ibara yake shahidi, ishirini ima zaidi, 
Uangaze ushahidi, maandiko ya Wadudi, 
Katu hawi mfisadi, kumukhimi wake Nabi. 

Na Musa wa Tauhidi, na Yeremia Mjudi, 
Manabii wa weledi, imara zao fuadi, 
Wakemea ufisadi, wa kafara za waladi, 
Haiwi kwa wetu Nabi, kumuasi wake Rabbi. 

Kumbukumbu la Torati, kumi na nane shahidi, 
Mistariye idadi, anza tisa na kuzidi, 
Na Yeremia mjudi, saba ndipo taka rudi, 
Thelathini na wahedi, mustari ndio budi. 

Kwa kaulize Wadudi, vitabuye vinanadi, 
Makafara ya waladi, ni machukizo ya kedi, 
Vipi wasema Wahabi, Katenda ya ufisadi, 
Kwani yake ni hududi, na mwingi wa ghufuradi. 

Kama mwenzetu wanadi., upagani itikadi, 
Za kuwatolea hadi, makafara ya waladi, 
Miungu yao ya jadi, Zeu, Herme na Wamedi, 
Simsingizie Nabi, katu si wa kuritadi. 

Bali mdi kwa mjadi, muasisi itikadi, 
Alofanya ukaidi, kuyapinga yalo hadi, 
Na kuleta yaso budi, alotoa kwa wajadi, 
Wakufuru na ya kedi, kusingizia Wadudi. 

Si kejeli wala kedi, ninakupa ushahidi, 
Kamrejee Luka (di), kama wewe u mweledi, 
Kwenye “Matendo” anadi, “Mungu – mtu”, Mungu jadi, 
Kumi na nne idadi, ibara kumi wahedi. 

Kwa nini  umwabe Yesu, “alofufuka” ni Zue, 
Au Herme, Adonisu, idadi yao ni kuu, 
Na Paulo ‘simsifu’, kwani mamboye makuu, 
Amewazuga lufufu, ya chini kufanya juu. 

Amechukua la Yesu, mbandikizia Zeu, 
Wafilipi kaarifu, sura ya pili nukuu, 
Ibara ya tano shufu, mpaka ya nane juu, 
Taona uharibifu, usijedhani nafuu, 
Simlazimishe Yesu, ukombozi wa “Wanguu”. 

Meno, 
S.L.P. 9409, 
Dar es Salaam. 
Utaratibu wa  kupa 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 

TAHARIRI 
Kuangukia makaa hakuna nafuu kwa aliye kikaangoni 

Wanawake Dodoma wataka mtoto aliyepigwa risasi akatibiwe nje 

Kesi za Mwembechai zaanza kusikilizwa 

Fitna ya Bakwata 

Dondoo za saikolojia: Tuonavyo mambo 

Waraka wa Baraza Kuu kuhusu Parole 

Inawezekana kufanyika mdahalo kati ya Waislamu na wasio Waislamu? 
Na Nandenga wa Mkomidachi 

Teknologia 
Jifunze Kuunganisha Kompyuta (2) 
Na Hassan Omar 

Serikali ihamie Dodoma kwanza ! 
Na. Said Rajab 

Mahafali ya AMSIR Iringa 
Na Mwandishi Wetu 

Madrasatul Nnajjary Islamiya 

Ijue Madrasatul Riyaadh 

Bihawana Sekondari wafungua Ijumaa 

Vijana Shinyanga watakiwa kuwa mfano mwema 
Na Jihad R. Saballa, Shinyanga 

Vyeo visiwasahaulishe majukumu yenu- Sheikh Abri 
Na Mwandishi Wetu, Iringa 

Jiandaeni na kifo – Sheikh Abdallah 
Na Mwandishi Wetu, Dodoma 

Semina zawazindua wanawake Bukoba 
Na Nadhiru Ishengoma 

Waislamu wanaomaliza Kidato cha Nne Tanga waaswa 
Na Ibn Mohamed 

Ndugu Kamuhabwa ndiye mwenye chuki na AN-NUUR 
Mwandishi: Maalim Bassalah 

'Ukombozi wa mwanamke si kugeuzwa biashara huria' 
Na Japhary Lemah, Arusha 

Polisi walinda amani katika muhadhara wa Wakristo 
Na Badru Kimwaga 

Mazengo wapewa uwanja wa kujenga Msikiti 
Na Mwandishi Wetu, Dodoma 

'Ajiengua Chuoni Z'bar kwa kutoruhusiwa kuvaa hijab' 
Na Seif Hamad Suleiman, Zanzibar 

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Shairi 
Simlazimishe Yesu ukombozi wa ulimwengu (jibu) 
 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita