|
|
Wanawake
Dodoma wataka mtoto aliyepigwa risasi akatibiwe nje
Wakiongea baada ya kongamano lao wanawake Waislamu wa mjini Dodoma wamesema itakuwa ni jambo la kushangaza wazazi kuwahangaikia watoto wao binafsi wapate elimu bora huku wakimwacha Chuki Athumani wodini kwa miezi tisa sasa. Walisema Chuki amedhulumiwa na ni lazima ndugu zake Waislamu na wananchi kwa ujumla wamsaidie kupata matibabu nje ya nchi ili ikiwezekana atembee kama alivyokuwa kabla ya kupigwa risasi na polisi. Awali katika kongamano hilo, maelfu ya wanawake hao Waislamu walilaani udhalimu waliofanyiwa Waislamu pale Mwembechai kwa kuuliwa kwa risasi za moto na wanawake kudhalilishwa. Wamehoji inakuwaje serikali idai ni ya uadilifu halafu ifumbie macho tendo la raia kuuliwa bila kosa tena kwa kulengwa shabaha "piga yule". Akiwakumbusha juu ya wajibu wao, mama Muslim aliwahimiza wanawake Waislamu kushikamana na vazi la hijaabu. Alisema mwanamke kutokuvaa hijaab anakuwa sawa na waya wa umeme usiovishwa kizuizi (insulator). Mama Muslim alisisitiza kwamba dawa ya ukimwi sio "mipira ya zinaa" bali kufuata sheria za Allah (sw). Alizitaja nchi za Waislamu kama Iran na Saudi Arabia ambapo athari ya ukimwi ni ndogo sana ikilinganishwa na sehemu nyingine duniani. Naye Bi. Ummy Salama aliwahimiza akina mama Waislamu washikamane katika kutafuta elimu, kujua haki zao, sheria na kuyajua mazingira yao kwa ujumla ili waweze kuifanya kazi ya Da’wah kwa ukamilifu. Ummy Salama aliwaonya vikali wanawake Waislamu wanaotafuta suluhisho la matatizo yao kwa kufuata kanuni za kitwaghuti. Aliwahimiza waisome Qur’an na waangalie masuala ya ndoa, talaka na mirathi. Kongamano hilo la wanawake Waislamu mjini Dodoma liliandaliwa na kikundi cha akina mama wa Kiislamu cha Bi. Khadija na kufanyika katika shule ya Al-Hijrah Oktoba 17, 1998. Wakati huo huo, Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu amesema kwamba tayari Baraza limemuandikia Waziri wa Afya Mh. Aron Chiduo ili atoe taratibu za kufuatwa na gharama za kumtibia mwanafunzi Chuki Athumani nchi za nje. Sheikh Kilima alisema kwamba kinachotakiwa ni mtoto Chuki kufanyiwa upasuaji na wataalamu wa mishipa ya fahamu (Neural Surgions) kwa tegemeo la kumuondolea kilema cha kulemaa. Aliwataka Waislamu na wananchi kwa ujumla kuwa tayari kutoa sadaka zao kumsaidia mtoto Chuki pindi Mh. Waziri atakapotoa gharama zinazohitajika. Hata hivyo taarifa ambazo AN-NUUR imezipata baadaye zimeeleza kwamba Wizara ya Afya kupitia barua yake No. HEC 426 ya Oktoba 22, 1998 imelielekeza Baraza Kuu kufuatilia taratibu za mtoto Chuki kutibiwa nje ya nchi huko huko Muhimbili. Haikuweza kufahamika mara moja ni kwanini Wizara ya Afya imechukua muda mrefu kiasi hicho kutoa maelekezo hayo. Maombi ya Baraza Kuu yalipelekwa kwa Mh. Waziri Chiduo tangu Julai 2,
1998.
|
YALIYOMO
TAHARIRI Kuangukia makaa hakuna nafuu kwa aliye kikaangoni Wanawake Dodoma wataka mtoto aliyepigwa risasi akatibiwe nje Kesi za Mwembechai zaanza kusikilizwa Dondoo za saikolojia: Tuonavyo mambo Waraka wa Baraza Kuu kuhusu Parole Inawezekana kufanyika mdahalo kati
ya Waislamu na wasio Waislamu?
Teknologia
Serikali ihamie Dodoma kwanza !
Mahafali ya AMSIR Iringa
Bihawana Sekondari wafungua Ijumaa Vijana Shinyanga watakiwa
kuwa mfano mwema
Vyeo visiwasahaulishe majukumu
yenu- Sheikh Abri
Jiandaeni na kifo – Sheikh
Abdallah
Semina zawazindua wanawake
Bukoba
Waislamu wanaomaliza Kidato
cha Nne Tanga waaswa
Ndugu Kamuhabwa ndiye mwenye
chuki na AN-NUUR
'Ukombozi wa mwanamke si kugeuzwa
biashara huria'
Polisi walinda amani katika
muhadhara wa Wakristo
Mazengo wapewa uwanja wa
kujenga Msikiti
'Ajiengua Chuoni Z'bar kwa
kutoruhusiwa kuvaa hijab'
Shairi
|