AN-NUUR
Na.167 Jamadul Awal 1419, Septembe 17 - 24, 1998

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita

 

Wanawake wakutana Mwanza na kusema:

Kunyanyaswa sasa basi

  • Wasema Damu iliyomwagika ilipwe
  • `Ipi nafasi ya Waislamu nchini hapa

Na Mwandishi Wetu, Mwanza'

WANAWAKE Waislamu waliokutana mjini Mwanza hivi karibuni wameungana na Waislamu wenzao kote nchini kuitaka serikali iwachukulie hatua waliohusika na mauaji ya Waislamu pale Mwembechai.

Wakihitimisha kongamano lao la siku moja, akina mama hao waliofurika katika Ukumbi wa Thaqaafa, waliitaka serikali ifanye kazi zake kwa uadilifu na sio kusema haina dini huku inaonyesha kwa uwazi kufanya upendeleo kwa misingi ya dini.

Wanawake hao waliwataka wanawake kote nchini watafakari nini wamejifunza na nini cha kufanya baada ya tukio la Mwembechai.

Aidha, wamewataka watafakari kwanini serikali imeridhia tendo la wanawake Waislamu kuvuliwa nguo na kupekuliwa na polisi wanaume wakati askari polisi na wale wa Magereza wapo wanawake. Ni upi unyanyasaji na udhalilishaji wa wanawake; wamehoji.

Kongamano hilo la aina yake mkoani Mwanza, lilifunguliwa kwa Qur'an tukufu iliyosomwa na Halima Issa ikifuatiwa na dua iliyosomwa na Hadija Omar.

Akina mama hao wapatao elfu moja na zaidi walijikuta wakiangua kilio pale walipokumbushwa mateso na vitendo vya kinyama walivyofanyiwa na polisi wanawake wenzao Msikitini Mwembechai na huko gerezani.

Katika kongamano hilo mabinti wawili walisilimu ambao ni Justina Emmanuel (Anglikana) ambaye alichagua jina la Mwanaidi na Upendo Nicholaus (Mkatoliki) aliyechagua jina la Fatma.

Juu 
 

YALIYOMO  
 
TAHARIRI 
Hakuna Muislamu aliyekufa kutokana na vurugu

Mgogoro wa kiwanja Duma: Wakatoliki wasema kuna njama za Waarabu Same Na Mwandishi Wetu

Wanawake wakutana Mwanza na kusema: Kunyanyaswa sasa basi
Na Mwandishi Wetu, Mwanza

Sheikh Omar Bashir ataka Waislamu waimarishe mshikamano
Na Said Sharif

Ustaadhi Abdallah Mfoyi afariki
Na Muhibu Saidi

Baraza Kuu halina Katibu Nguruka - Sheikh Kilima
Na Abu Adli

Viongozi Msikiti wa Ubungo Darajani waitwa polisi
Na Kassim Juma

Marekani `ilivyosaidia' Mujahidiin

Barua ya mtoto wa miaka minne toka Lebanon kwa Bibi Hillary Clinton

Ujumbe wa waandishi kwa Bw. Batendi, Wakristo
Na Muhibu Saidi

Waislamu wanadhalilishwa au wanajidhalilisha

Tusiwe Jogoo wa Esopo na Almasi
Na MAALIM ALI BASSALEH

Sherehe za wiki ya usalama barabarani: Kauli nzito za waheshimiwa zimekalia kuti kavu
Na Said Omar

Mwanasayansi Avicenna: Tabibu bingwa.
Na Dk. A. A. Amur

Ujenzi wa Msikiti wa Ijumaa Mriti waanza
Na Nasib A. Mziray

Kutoweka kwa hazina adimu za kimazingira
Na Yassir Salim

Mfalme Najashi ni mfano bora wa kuigwa kwa watawala
Na Idi Kikong'ona

Waislamu Moro wasaidia wagonjwa
Na Mwandishi Wetu, Morogoro

KUFUATIA KUTISHIA MAGAZETI: Sheikh Ayoub amjibu Askofu Rajab Rajab
Na Mussa Ally

TAMSA Tanga waahidi kuendeleza mema
Na Ibn Mohammed, Tanga

Ufugaji, uuzaji nguruwe wakera wananchi Dar
Na Mwandishi Wetu

Mafundisho ya Quran 
Kuwepo kwa ufufuo

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Haja ya maji ya kunywa

 

 

 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org  

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita