AN-NUUR
Na.167 Jamadul Awal 1419, Septembe 17 - 24, 1998

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita

 

Mgogoro wa kiwanja Duma:

Wakatoliki wasema kuna njama za Waarabu Same

  • Wadai `watavamiwa' na Iran, Iraq, Somalia na Zanzibar
  • Waogopa kuzuiwa kufuga nguruwe

Na Mwandishi Wetu

HABARI kutoka Duma wilayani Same zimeeleza kwamba Wakatoliki wamepinga hukumu ya mahakama ya mwanzo iliyowapa ushindi Waislamu katika Shauri la Madai No. 63/98.

Katika kupinga kwao hukumu hiyo Wakatoliki wamedai kwamba wana ushahidi kwamba Waislamu wamepatiwa fedha kutoka Iran, Iraq, Somalia na Zanzibar.

Aidha, wameitaka mahakama ilipe uzito dai lao la kutengua ushindi wa Waislamu kwa madai kwamba tayari eneo hilo linatembelewa na Waarabu.

Wamedai kwamba kuja kwa Waarabu hao kumewapa wasiwasi Wakatoliki kwamba huenda Waarabu wanayo njama fulani huko Duma.

Pamoja na maelezo hayo, habari kutoka Duma zimeeleza kwamba Wakatoliki katika moja ya sababu zao za kukata rufaa, wamedai kwamba Waislamu wamewatishia kuwahamisha kwa vile wanafuga nguruwe.

Waislamu walitakiwa na mahakama ya wilaya kwamba wawe wameshajibu hoja hizo za Wakatoliki pamoja na nyingine zilizowasilishwa mahakamani Septemba 1I, mwaka huu.

Hata hivyo, Waislamu wameiomba mahakama hiyo iwape muda zaidi na sasa Shauri litatajwa Oktoba 2, 1998.

Katika Shauri hilo, Waislamu walidai kwamba Wakatoliki walikuwa wamevamia eneo lao la Msikiti na shule walilopewa toka mwaka 1953.

Julai 30, mwaka huu mahakama ya mwanzo Same ilitoa hukumu kwamba eneo linalolalamikiwa ni la Waislamu na Wakatoliki waliamriwa kulipa fidia ya miti waliyokata.

Juu 
 

YALIYOMO  
 
TAHARIRI 
Hakuna Muislamu aliyekufa kutokana na vurugu

Mgogoro wa kiwanja Duma: Wakatoliki wasema kuna njama za Waarabu Same Na Mwandishi Wetu

Wanawake wakutana Mwanza na kusema: Kunyanyaswa sasa basi
Na Mwandishi Wetu, Mwanza

Sheikh Omar Bashir ataka Waislamu waimarishe mshikamano
Na Said Sharif

Ustaadhi Abdallah Mfoyi afariki
Na Muhibu Saidi

Baraza Kuu halina Katibu Nguruka - Sheikh Kilima
Na Abu Adli

Viongozi Msikiti wa Ubungo Darajani waitwa polisi
Na Kassim Juma

Marekani `ilivyosaidia' Mujahidiin

Barua ya mtoto wa miaka minne toka Lebanon kwa Bibi Hillary Clinton

Ujumbe wa waandishi kwa Bw. Batendi, Wakristo
Na Muhibu Saidi

Waislamu wanadhalilishwa au wanajidhalilisha

Tusiwe Jogoo wa Esopo na Almasi
Na MAALIM ALI BASSALEH

Sherehe za wiki ya usalama barabarani: Kauli nzito za waheshimiwa zimekalia kuti kavu
Na Said Omar

Mwanasayansi Avicenna: Tabibu bingwa.
Na Dk. A. A. Amur

Ujenzi wa Msikiti wa Ijumaa Mriti waanza
Na Nasib A. Mziray

Kutoweka kwa hazina adimu za kimazingira
Na Yassir Salim

Mfalme Najashi ni mfano bora wa kuigwa kwa watawala
Na Idi Kikong'ona

Waislamu Moro wasaidia wagonjwa
Na Mwandishi Wetu, Morogoro

KUFUATIA KUTISHIA MAGAZETI: Sheikh Ayoub amjibu Askofu Rajab Rajab
Na Mussa Ally

TAMSA Tanga waahidi kuendeleza mema
Na Ibn Mohammed, Tanga

Ufugaji, uuzaji nguruwe wakera wananchi Dar
Na Mwandishi Wetu

Mafundisho ya Quran 
Kuwepo kwa ufufuo

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Haja ya maji ya kunywa

 

 

 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org  

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita