|
|
|
Aya ya 264 "Enyi mlioamini! Msiharibu sadaka zenu kwa masimbulizi na udhia, kama yule anayetoa mali yake kwa kuwaonyesha watu, wala hamuamini Allah wala siku ya mwisho. Basi hali yake ni kama hali ya jabali ambalo juu yake pana udongo, kisha ikalifikia mvua kubwa na ikaliacha tupu. Basi hawatakuwa na uweza (wa kupata) chochote katika walivyovichuma; na Allah hawaongozi watu makafiri". Hapa Allah analinganisha masimbulizi na udhia katika kutoa mali kuwa ni sawa na riya ile kutoa kwa ajili ya kujionyesha kwa wanadamu wengine na siyo kwa kutaka radhi za Allah. Hii ni picha halisi ya unafiki na utendaji wa wanafiki kwani sifa yao kuu ni kushindwa kuoanisha kati ya nia (yale yaliyo moyoni) na yale yanayotokea nje ya moyo wake na hivyo kuthibitisha kauli ya Allah kuwa hawa si watu wenye kuamini. Tendo la kutoa kinafiki siku zote ni la hatari na lisilo na manufaa yoyote kwa mtoaji wala kwa yule anayepewa. Ni kwa sababu hiyo, Allah akatoa mfano wa utoaji huo kulingana na mvua inayonyesha juu ya jabali lililofunikwa na mchanga kidogo juu yake ambao kwa kawaida hapana kitu kinachoweza kuota juu yake. Kutoa katika njia ya Allah kumelinganishwa au kupigiwa mfano wa mvua katika aya hii wakati jabali limefananishwa na ile nia mbaya ya kutoa kwa nia au kutoa na baadaye kufuatisha masimango. Mchanga kidogo ulio juu ya jabali ni sawa na ile picha wanayoipata wanadamu wengine ambao hawajui nia ya mtoaji kwani imefichika moyoni. Kikawaida mvua inaponyesha hutegemewa kuleta manufaa kwenye ardhi na hatimaye kwa wanadamu ambao wanaitumia ardhi hiyo kwa shughuli mbalimbali zikiwemo zile za kilimo. Hata hivyo, jambo hilo halitokei wakati mvua inapoanguka kwenye jabali lenye mchanga na kuliwacha jabali tupu ambalo halioteshi mmea wowote. Kitendo cha utoaji kinategemewa kiongeze hisia za wema au ucha Mungu kwa mtoaji lakini inapokosekana nia nzuri huwa hakina manufaa sawa na mvua inyeshayo juu ya jabali tu. Kwa lugha nyingine mali itolewayo kinyume na maagizo ya Allah haitofautiani na mali inayofisidiwa kwa mtoaji zaidi ya kuiharibu hiyo mali yenyewe. Aya inamalizia kuwataja watu hao wanaotoa kwa malengo mengine yasiyo ya kupata fadhila za Allah kama makafiri. Kafiri kwa hapa ni mtu asiye na shukrani au kukubali utoaji kwa lengo la radhi za Allah. Mtu huyu hastahili kuongozwa na Allah kwani hana anachokifanya kwa kutaraji
chochote kutoka kwake hivyo ameachiwa aende atakako.
|
YALIYOMO
TAHARIRI
Waislamu wasisitiza: Nyumba ya Waziri
Mkuu ni ya Waislamu
Kuchomwa nyumba za wananchi
Maoni Yetu:
Nguruwe marufuku Kinondoni – Tume
Watanzania waanzisha Baraza la Waislamu
Marekani
Wanawake Hai wamtaka Rais azungumzie
mauaji ya Mwembechai
‘Serikali haiwezi kuzuia rushwa’
Makala ya Kimataifa
Afghanistan washindi dhidi
ya uvamizi karne zote
MAKALA:
Tujikwamue na janga la utwaghuti
MAONI:
MAKALA:
Tufuate Uislamu kwa vitendo
na siyo kwa maneno -2
Tusihalalishe mauaji ya
raia kwa kisingizio cha ‘wananchi wenye hasira’
Historia ya sayansi na tiba
Msiwageuze watoto ombaomba
MAKALA YA JAMII:
Sensa ya majaribio: Wananchi watofautiana
na serikali
Uislamu ulivyoingia Zanzibar -3 Mwembechai wageuka Hame,
Bado walindwa na polisi
Waislamu Moro waendelea kusaidia
wagonjwa
Mjadala wa Katiba ya Shirikisho
kuzinduliwa Dar Jumapili
Walimu wa dini Tanga wapokea
Baiskeli
Mafundisho ya Quran
Chakula na Lishe
|