AN-NUUR 
Na.170 Jamadul Akhir 1419, Oktoba 9 - 15, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 
Mafundisho ya Qur’an
Kutoa katika njia ya Allah

Aya ya 264 

"Enyi mlioamini! Msiharibu sadaka zenu kwa masimbulizi na udhia, kama yule anayetoa mali yake kwa kuwaonyesha watu, wala hamuamini Allah wala siku ya mwisho. Basi hali yake ni kama hali ya jabali ambalo juu yake pana udongo, kisha ikalifikia mvua kubwa na ikaliacha tupu. Basi hawatakuwa na uweza (wa kupata) chochote katika walivyovichuma; na Allah hawaongozi watu makafiri". 

Hapa Allah analinganisha masimbulizi na udhia katika kutoa mali kuwa ni sawa na riya ile kutoa kwa ajili ya kujionyesha kwa wanadamu wengine na siyo kwa kutaka radhi za Allah. Hii ni picha halisi ya unafiki na utendaji wa wanafiki kwani sifa yao kuu ni kushindwa kuoanisha kati ya nia (yale yaliyo moyoni) na yale yanayotokea nje ya moyo wake na hivyo kuthibitisha kauli ya Allah kuwa hawa si watu wenye kuamini. 

Tendo la kutoa kinafiki siku zote ni la hatari na lisilo na manufaa yoyote kwa mtoaji wala kwa yule anayepewa. Ni kwa sababu hiyo, Allah akatoa mfano wa utoaji huo kulingana na mvua inayonyesha juu ya jabali lililofunikwa na mchanga kidogo juu yake ambao kwa kawaida hapana kitu kinachoweza kuota juu yake. 

Kutoa katika njia ya Allah kumelinganishwa au kupigiwa mfano wa mvua katika aya hii wakati jabali limefananishwa na ile nia mbaya ya kutoa kwa nia au kutoa na baadaye kufuatisha masimango. 

Mchanga kidogo ulio juu ya jabali ni sawa na ile picha wanayoipata wanadamu wengine ambao hawajui nia ya mtoaji kwani imefichika moyoni. 

Kikawaida mvua inaponyesha hutegemewa kuleta manufaa kwenye ardhi na hatimaye kwa wanadamu ambao wanaitumia ardhi hiyo kwa shughuli mbalimbali zikiwemo zile za kilimo. 

Hata hivyo, jambo hilo halitokei wakati mvua inapoanguka kwenye jabali lenye mchanga na kuliwacha jabali tupu ambalo halioteshi mmea wowote. 

Kitendo cha utoaji kinategemewa kiongeze hisia za wema au ucha Mungu kwa mtoaji lakini inapokosekana nia nzuri huwa hakina manufaa sawa na mvua inyeshayo juu ya jabali tu. 

Kwa lugha nyingine mali itolewayo kinyume na maagizo ya Allah haitofautiani na mali inayofisidiwa kwa mtoaji zaidi ya kuiharibu hiyo mali yenyewe. 

Aya inamalizia kuwataja watu hao wanaotoa kwa malengo mengine yasiyo ya kupata fadhila za Allah kama makafiri. Kafiri kwa hapa ni mtu asiye na shukrani au kukubali utoaji kwa lengo la radhi za Allah. 

Mtu huyu hastahili kuongozwa na Allah kwani hana anachokifanya kwa kutaraji chochote kutoka kwake hivyo ameachiwa aende atakako. 
 
Juu 
 

YALIYOMO 
 
 

TAHARIRI 
Tutaendelea kudhalilishwa mpaka lini ? 

Waislamu wasisitiza: Nyumba ya Waziri Mkuu ni ya Waislamu 
Na Mwandishi Wetu 

Kuchomwa nyumba za wananchi 
Na Mwandishi wetu 

Maoni Yetu: 
Maisha ya Mtanzania yanapokosa thamani 

Nguruwe marufuku Kinondoni – Tume 
Na Kassim Juma 

Watanzania waanzisha Baraza la Waislamu Marekani 
Na Mwandishi Wetu 

Wanawake Hai wamtaka Rais azungumzie mauaji ya Mwembechai 
Na Mwandishi Wetu 

‘Serikali haiwezi kuzuia rushwa’ 
Na Kassim Msuya 

Makala ya Kimataifa 
Nani gaidi: Slobodan Milosovic au Usama bin Laden 
Na Mwandishi Wetu 

Afghanistan washindi dhidi ya uvamizi karne zote 
Na Faiza bint Abubaka 

MAKALA: 
Demokrasia ya rushwa ! 
Na Mwapwani Mohamed 

Tujikwamue na janga la utwaghuti 
Na I. Kikong’ona 

MAONI: 
Nini Jihad na nani Mujahidina ? 

MAKALA: 
Marekani ni magaidi wa haki za binadamu 
Na MUSSA ALLY 

Tufuate Uislamu kwa vitendo na siyo kwa maneno -2 
Mwandishi: Maalim Ali Bassaleh 

Tusihalalishe mauaji ya raia kwa kisingizio cha ‘wananchi wenye hasira’ 
Na Mwandishi Wetu 

Historia ya sayansi na tiba 
Na Dk. Amur A.A. 

Msiwageuze watoto ombaomba 
Na H.E. Omar 

MAKALA YA JAMII: 
Profesa Malise Kaisi acha uzushi dhidi ya Mtume Muhammad 

Sensa ya majaribio: Wananchi watofautiana na serikali 
Na Rajab Rajab - Morogoro 

Uislamu ulivyoingia Zanzibar -3 

Mwembechai wageuka Hame, Bado walindwa na polisi 
Na Badru Kimwaga 

Waislamu Moro waendelea kusaidia wagonjwa 
Na Rajab Rajab - Morogoro 

Mjadala wa Katiba ya Shirikisho kuzinduliwa Dar Jumapili 
Na Mohamed Othman 

Walimu wa dini Tanga wapokea Baiskeli 
Na Abu Said 

Mafundisho ya Quran 
Kutoa katika njia ya Allah: Al-Baqarah aya  264 

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Vitu vinavyoweza kuwemo katika vyakula 

  

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita