|
|
WAISLAMU wamesisitiza kwamba nyumba iliyochukuliwa na Waziri Mkuu ni ya Waislamu na inapaswa kurejeshwa kwa wenyewe. Pamoja na kuirejesha, Waislamu wamedai kwamba ni lazima serikali ilipe malimbikizo ya kodi toka ilipoipora nyumba hiyo mwaka 1971. Waislamu mbalimbali walioongea na mwandishi wa habari hizi wamesema kwamba zipo nyumba zipatazo 11 za Waislamu katika maeneo ya Upanga n Oysterbay ambazo zimechukuliwa na serikali kinyume cha sheria. Moja ya nyumba hizo ni ile iliyopo Oysterbay Plot No. 11 barabara ya Tumbawe ambayo imechukuliwa na Waziri Mkuu. Awali, nyumba hiyo ilikuwa mali ya Ali Dewji Gangji wa Singida na baadaye kukabidhiwa East African Muslim Welfare Society (EAMWS) ambapo EAMWS ilipovunjwa Kabidhi Wasia Mkuu alikabidhi hati ya nyumba hiyo kwa Bakwata. Hata hivyo, imeelezwa kwamba nyumba hiyo pamoja na nyingine zilitaifishwa na serikali mwaka 1971 kinyume cha sheria. Mwenyekiti wa Kamati ya Nyumba za Bakwata Sheikh Yahya Hussein amesema kwamba katika nyumba 11 za Waislamu zilizopo eneo la Upanga ambazo zimeporwa na serikali ni nyumba mbili tu ambazo Bakwata imefanikiwa kuzipata kupitia msaada wa Mh. Mzee Rashid Kawawa. Sheikh Yahya Hussein amesema kwamba zaidi ya nyumba hizo 9, kipo kiwanja cha Waislamu kilichopo kona ya Mitaa ya Mkunguni Bibi Titi na Morogoro Road ambacho kimeporwa na kupewa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC). Amesema kazi kubwa ya Kamati yake hivi sasa ni kuhakikisha kwamba serikali inazirejesha mali za Waislamu ili mali hizo ziweze kutumiwa katika namna ile ile iliyokusudiwa na wale waliotoa Waqf. Zipo taarifa kutoka Wizara ya Sheria na Mambo ya Katiba kwamba serikali inataka kuilipa Bakwata fidia ili ichukue nyumba hiyo iwe ya Waziri Mkuu. Hata hivyo, Waislamu hadhaa waliobahatika kuongea na mwandishi wa habari hizi, wamesisitiza kwamba jambo hilo haliwezi kukubalika. Kiongozi mmoja ndani ya Bakwata ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini
amesema kwamba nyumba hiyo haiwezi kuuzwa. Bali serikali kwanza ilipe malimbikizo
ya kodi na kama Waziri Mkuu anaiependa basi aingie mkataba na Bakwata apangishwe.
|
YALIYOMO
TAHARIRI
Waislamu wasisitiza: Nyumba ya Waziri
Mkuu ni ya Waislamu
Kuchomwa nyumba za wananchi
Maoni Yetu:
Nguruwe marufuku Kinondoni – Tume
Watanzania waanzisha Baraza la Waislamu
Marekani
Wanawake Hai wamtaka Rais azungumzie
mauaji ya Mwembechai
‘Serikali haiwezi kuzuia rushwa’
Makala ya Kimataifa
Afghanistan washindi dhidi
ya uvamizi karne zote
MAKALA:
Tujikwamue na janga la utwaghuti
MAONI:
MAKALA:
Tufuate Uislamu kwa vitendo
na siyo kwa maneno -2
Tusihalalishe mauaji ya
raia kwa kisingizio cha ‘wananchi wenye hasira’
Historia ya sayansi na tiba
Msiwageuze watoto ombaomba
MAKALA YA JAMII:
Sensa ya majaribio: Wananchi watofautiana
na serikali
Uislamu ulivyoingia Zanzibar -3 Mwembechai wageuka Hame,
Bado walindwa na polisi
Waislamu Moro waendelea kusaidia
wagonjwa
Mjadala wa Katiba ya Shirikisho
kuzinduliwa Dar Jumapili
Walimu wa dini Tanga wapokea
Baiskeli
Mafundisho ya Quran
Chakula na Lishe
|