AN-NUUR 
Na.175 Rajab 1419, Novemba 13 - 19, 1998 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Wazo mpachiko
(Programmed mind)
 
Na Abu Halima Sa Changwa

WAZO mpachiko ni wazo linalopachikwa katika akili ya mtu hadi linakuwa ni sehemu ya dhana au imani ya mtu huyo. Mara nyingi wanaopachika watu mawazo huwapachika wakiwa wadogo, na kuhakikisha kuwa wanaopachikwa wanakuwa (kiumri) na wazo hilo. Inawezekana pia kwa mtu mzima kupachikwa wazo. 

Mfano mzuri wa wazo mpachiko ni lile wazo waliopachikwa watu wakawa na dhana ya kumuona tajiri kama mtu mbaya, na kumwita bepari, mlanguzi, kupe, bwanyenye na kadhalika, hadi watu wakaogopa kuwa matajiri. Kwa jinsi utajiri ulivyochukuliwa kama ni dhambi, baadhi ya "watuhumiwa" walidiriki hata kutupa mali zao baharini. 

Mara nyingine mtu huweza kugundua kirahisi tu kuwa wazo alilonalo ni mpachiko, na huliacha, kama halina mantiki. Kwa mfano, wengi tulipachikwa dhana kuwa ukimuona mama yako ana mtoto mchanga, basi ujue kanunua, labda dukani, sokoni au hospitali, au kamuokota. Baadaye, dhana hii hutoweka na tunatokea kujua watoto wanavyopatikana. 

Leo ninaleta wazo mpachiko lililowajaa mamilioni ya watu, wengine ni maprofesa wenzangu. Hebu angalia picha iliyopo hapo. Wengi wetu tunamuona mtu aliyelala chali akiwa yuko uchi. Pengine wasomaji wengi watashangaa kwa nini Sa Changwa leo kaweka picha mbaya ya mtu ambaye hajajistiri. Sina ajenda ya siri naomba univumilie kidogo. 

Angalia nukta zilizowekwa kuizunguka picha hiyo, halafu chukua kalamu uchore mistari kuunganisha nuka moja hadi nyingine kwa mfuatano wa namba, kuanzia moja, mbili, tatu na kuendelea. Hapo utagundua kwamba dhana ya mwendauchi aliyelala chali inaondoka, inakuja dhana ya mtu mtakatifu, ambaye wengi humwita mwokozi. Dhana hii ya pili ikishakuja, kwa wengi ile dhana ya mtu katundikwa kwenye mbao akiwa uchi inaondoka. Kwa wengine, mwendauchi yule hubadilika kuwa mungu wao. 

Kwa wale wenzangu wanaoamini kuwa kufufuka kupo, tujaribu kupiga picha, huyu jamaa akifufuka, halafu akakuta masanamu na picha zake akiwa katundikwa, yuko uchi, karaliwa shingoni, na anaitwa mungu, hivi atajisikiaje? 

Ili kutuweka huru na wazo hili mpachiko, Mwenyezi Mungu anatumbia: 

"Na hawakumuua wala hawakumsulubu..." (Qur. 4:157) 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Maoni  
Kuvuja kwa mitihani: Tuweni wakweli kwa nchi yetu  

Katibu wa Baraza Kuu  azikwa Dar  
Na Mwandishi Wetu  

Ubabe wa madhalimu kuzimwa:  
Na Mwandishi Wetu  

MACHO YA SHUTUMA  
Na Abu Halima Sa Changwa  

Wazo mpachiko (Programmed mind)  
Na Abu Halima Sa Changwa  

Ta'azia: Abbas Shaaban Kilima 1938-1998  

Wasemavyo Wanaharakati  

Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo- 4  
Na Nandenga wa Mkomidachi  

Siri ya Miujiza  
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa  

Umuhimu wa Elimu ya Awali kwa watoto wadogo  
Na Ustaadh Kupa Pazi Said  

Ifahamu Madrasat Ghazal Muslim - Moro  
Na Mussa Ally, Morogoro  

Pamoja na sala, tusimamishe zakah  
Na Abubakari S. Marwillo  

Aina za maudhi yaliyoharamishwa juu ya Muislamu  
Na. Ramla  

Israi na Miiraji ni miujiza  
Mwandishi: Maalim Bassaleh  

Pamoja na ahadi ya Serikali kuzifuta: kesi za mihadhara zaendelea mahakamani  
Na Muhibu Said  

Waislamu Uluguruni  Moro wazama kwenye matambiko  

Imarisheni miradi ya elimu -  Prof.  Mikidadi  
Na Mwandishi Wetu, Dodoma  

Teknologia: Jifunze Kuunganisha Kompyuta (5)  
Na Hassan Omar  

Mafunzo ya Qur'an  
Shetani anawaogopesha wenye mali kutoa  

Chakula na lishe  
[Kansa ya tumbo]  

Matangazo  
 
 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita